SHEIKH NASSOR AWAONYA VIJANA KUHUSU UVUNJIFU WA AMANI
Автор: CALES TV
Загружено: 2025-11-16
Просмотров: 548
Описание:
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Alhaji Issa Nassor, amewataka vijana mkoani humo kuepuka kushiriki katika vitendo vyovyote vinavyohatarisha au kuvunja amani ya nchi. Amesema baadhi ya taarifa na maneno yanayoenea kupitia mitandao ya kijamii yamekuwa chanzo cha chuki, taharuki na kupotosha ukweli kuhusu viongozi wa taifa, hivyo vijana wanapaswa kuwa waangalifu na kuepuka kuyafuata bila kujiridhisha.
Akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu katika mji mdogo wa Nduguti, wilayani Mkalama, Sheikh Nassor amesema amani ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa, hivyo kila kijana anapaswa kuwa mlinzi wa amani na mshiriki wa juhudi za kudumisha umoja na mshikamano. Aidha, amesisitiza kuwa viongozi wa dini wanaendelea kuhimiza maadili, upendo na utiifu kwa mamlaka halali za nchi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: