VIONGOZI RUSESA WAPINGA UAMUZI WA KUHAMISHA SHULE, WASEMA WANANCHI HAWAKUSHIRIKISHWA
Автор: STARBORN PICTURES
Загружено: 2026-01-20
Просмотров: 166
Описание:
Viongozi wa Kata ya Rusesa wameeleza kulalamikia uamuzi wa Serikali wa kuhamisha shule iliyopo katika kata hiyo bila kushirikisha wala kusikiliza maoni ya wananchi husika.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi hao wamesema kuwa uamuzi huo umeibua maswali na sintofahamu kubwa miongoni mwa wakazi wa eneo hilo, wakidai kuwa shule hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya elimu ya watoto wao.
Wananchi wamesisitiza kuwa hawakushirikishwa katika hatua yoyote ya maamuzi, jambo ambalo linakwenda kinyume na misingi ya utawala bora na ushirikishwaji wa jamii. Viongozi hao wameiomba Serikali kupitia upya uamuzi huo na kutoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni yao kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.
Endelea kufuatilia taarifa hii kwa undani zaidi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: