TADB, Sivat Agribusiness na Wafugaji wadogo wanavyoshirikiana kuongeza thamani ya maziwa Arumeru
Автор: tadbtz
Загружено: 2025-08-08
Просмотров: 260
Описание:
Sivat Agribusiness ni kiwanda cha kuchakata maziwa kilichopo Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha, kinachofanya kazi kwa karibu na wafugaji wadogo ili kuongeza thamani katika mnyororo wa maziwa hapa Tanzania.
Kupitia uwezeshaji wa kifedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Sivat imeweza kuwekeza kwenye mitambo ya kisasa ya kuchakata maziwa na miundombinu ya baridi ya kuhifadhi maziwa, hatua iliyoboreshwa ubora, usalama na muda wa matumizi wa bidhaa za maziwa.
Kwa kununua maziwa moja kwa moja kutoka kwa wafugaji wadogo, kuyachakata kuwa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu, na kuyasambaza sokoni, Sivat inaongeza thamani katika kila hatua ya mnyororo wa uzalishaji.
Ushirikiano huu umefungua fursa kwa wafugaji kupata soko la uhakika, bei bora, na malipo ya wakati ikiwa ni mfano bora wa jinsi uwezeshaji wa kilimo-biashara unavyoweza kuleta mabadiliko ya kweli katika maisha ya wakulima na wafugaji wadogo nchini.
#TADB #kilimokinabenkika #miaka10yamabadiliko #10yearsoftransformation #dairyfarm #dairy #dairymilk #TI3P #sivat #KilimoBiashara #SektaYaMaziwa #UwezeshajiVijana #10YearsOfTADB
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: