Wanufaika wa TADB Kagera Wapata Soko la Uhakika Kupitia Kahama Fresh
Автор: tadbtz
Загружено: 2025-08-07
Просмотров: 265
Описание:
Kupitia uwezeshaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), kiwanda cha Kahama Fresh kimekuwa mkombozi kwa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa mkoani Kagera.
Mtandao wa vituo vya ukusanyaji maziwa, wafugaji waliopata mikopo kutoka TADB sasa wanapata soko la uhakika la kuuza maziwa yao kila siku kwa bei nzuri na kwa wakati.
Ushirikiano huu baina ya TADB na Kahama Fresh umeleta mapinduzi ya kweli. Watu wengi zaidi sasa wamehamasika kuwekeza katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kutokana na kuaminika kwa soko. Hii imechochea ongezeko la uzalishaji, kipato kwa kaya, na ukuaji wa uchumi wa ndani.
Kahama Fresh si tu mnunuzi, bali ni mshirika wa maendeleo. Kwa pamoja na TADB, wamejenga mnyororo imara wa thamani unaoleta mabadiliko chanya kwa jamii: kuunda ajira, kukuza kilimo-biashara, na kuimarisha maisha ya wafugaji wa Kagera.
#TADB #kilimokinabenkika #miaka10yamabadiliko #10yearsoftransformation #dairyfarm #dairy #dairymilk #TI3P #KahamaFresh #KilimoBiashara #SektaYaMaziwa #UwezeshajiVijana #10YearsOfTADB
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: