MBUNGE MAFUWE AIBUA KERO YA UCHELEWESHAJI WA UHAMISHO KWA WALIMU NA WATUMISHI
Автор: TZA MEDIA HUB
Загружено: 2025-06-23
Просмотров: 311
Описание:
Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe, leo ameibua hoja nzito kuhusu ucheleweshaji wa uhamisho kwa walimu na watumishi wengine wa umma, akisema hali hiyo imekuwa kero kubwa kwa watumishi wanaokamilisha taratibu zote lakini wanacheleweshwa kuhamishwa kutoka vituo vya kazi.
Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bungeni jijini Dodoma, Mafuwe alieleza kuwa kuna walimu na watumishi waliomaliza mchakato wa uhamisho kwa mujibu wa taratibu, lakini wanabaki kwenye vituo vyao kwa miezi au hata miaka wakisubiri majibu yasiyo na uhakika.
“Mtumishi anakuwa ameshamaliza kila kitu, lakini anabaki tu kwenye kituo akisubiri majibu. Hili ni jambo linaloumiza na linapaswa kushughulikiwa kwa haraka,” alisema Mafuwe.
Katika majibu yake, Serikali kupitia Ofisi ya Rais - Utumishi na Utawala Bora, ilieleza kuwa mfumo wa sasa wa uhamisho kwa walimu na watumishi wengine wa umma kupitia Electronic Complaints and Compliments (ECC) umeshafanyiwa maboresho ili kuharakisha uamuzi wa uhamisho.
“Katika mfumo wa ECC, ikiwa mtumishi ameomba uhamisho na msimamizi wake (supervisor) hatatoa majibu ndani ya muda, ombi hilo sasa litapelekwa moja kwa moja kwenye ngazi ya juu kwa ajili ya uamuzi,” ilieleza Serikali.
Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa maombi ya uhamisho hayatokwama kwenye ngazi ya wakuu wa vituo au waajiri wa moja kwa moja, hali ambayo imekuwa ikichangia malalamiko ya kucheleweshwa kwa watumishi katika kupata majibu.
Wadau wa elimu na utumishi wamepongeza hatua hiyo ya serikali, wakisema itasaidia kupunguza msongamano wa maombi na kurudisha ari ya watumishi waliokuwa wakikata tamaa kutokana na kucheleweshwa kwa majibu ya uhamisho bila sababu za msingi.
Mwisho
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: