MBUNGE AAHIDI KUOGA HADHARANI MRADI WA MAJI UKIKAMILIKA
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2025-02-23
Просмотров: 722
Описание:
Mbunge wa Handeni Mjini, Kwagilwa Ruben, ameahidi kuoga hadharani baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Akizungumza mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyeanza ziara yake ya kikazi mkoani humo leo Jumapili, Februari 23, 2025, Ruben amesema mradi huo utakapokamilika na maji kuanza kutiririka, atatekeleza ahadi yake kama ishara ya furaha kwa wananchi waliokuwa na changamoto ya upatikanaji wa maji kwa muda mrefu.
" Mheshimiwa Rais, kwa furaha niliyonayo, siku maji yatakapotiririka baada ya mradi huu mkubwa kukamilika, nimewaahidi wananchi hawa kuwa nitaoga hadharani! Hata hivyo, hicho mnachosubiri kukiona hamtakiona maana nitaoga na nguo," amesema Ruben akiwachangamsha wananchi.
Video na Khatibu Mgeja.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: