MAWAKILI ZANZIBAR WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA USAJILI WA NYARAKA NA MALI
Автор: ASAM Online TV
Загружено: 2026-03-07
Просмотров: 125
Описание:
Mawakili wa Zanzibar wametakiwa kuwa makini katika kusajili nyaraka na mali pamoja na kufuata sheria zote za usajili ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza katika jamii.
Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara, Ndugu Seif Mohammed alipokuwa akifungua warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Business and Property Registration Agency (BPRA).
Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil, Kikwajuni, Mkoa wa Mjini Magharibi, na imewakutanisha mawakili pamoja na wataalamu mbalimbali wa masuala ya sheria na usajili wa mali.
Akizungumza katika ufunguzi wa warsha hiyo, Ndugu Seif amesema ni muhimu kwa kila mwanasheria kuzingatia taratibu na misingi ya sheria katika kazi zao ili kuhakikisha sheria zinafuatwa kikamilifu, jambo litakalosaidia kuimarisha utendaji wao na kuleta ufanisi pamoja na utulivu katika sekta hiyo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa BPRA, Ndugu Khamis Juma Khamis amesema taasisi hiyo imeamua kuwakutanisha mawakili na wasomi mbalimbali kwa lengo la kuwapatia elimu kuhusu sheria na kanuni za usajili wa nyaraka na mali.
Ameeleza kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza uelewa kwa wataalamu hao ili waweze kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria pamoja na kutumia mifumo ya kisasa ya kielektroniki katika utekelezaji wa majukumu yao.
Nao baadhi ya mawakili walioshiriki katika warsha hiyo wameipongeza BPRA kwa kuandaa mkutano huo, wakisema utawasaidia kuongeza uelewa wa sheria na kuimarisha utendaji wao wa kazi badala ya kufanya kazi kwa mazoea.
#ASAMOnlineTV
#BPRA
#SheriaNaUsajili
#Zanzibar
#UtawalaBora
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: