BASHUNGWA AMUONDOA MENEJA WA TANROADS MKOA WA LINDI, MTAALAM WA FALSAFA AKUTWA 'SITE' AKISIMAMIA..
Автор: Wizara ya Ujenzi
Загружено: 2024-03-06
Просмотров: 19481
Описание:
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemsimamisha kazi Meneja wa TANROADS Mkoa wa Lindi, Eng. Andrea Kasamwa kwa kushindwa kusimamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara na madaraja katika Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi na kupelekea barabara kuu zinanounganisha wilaya hiyo na maeneo mengine kufungwa.
Waziri Bashungwa akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Deo Ndejembi ameshuhudia urejeshwaji wa barabara ya Liwale - Nangurukuru iliyosombwa na maji ikisimamiwa na Mtaalam mwenye taaluma ya Falsafa kwa kusaidiwa na Wananchi wakati Mkandarasi akiwa hayupo eneo la Kazi.
Bashungwa amechukua hatua hiyo leo tarehe 06 Machi 2024 wakati akikagua mindombinu ya barabara katika Wilaya ya Liwale na kutoridhishwa na usimamizi wa kazi inayofanywa na Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Lindi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: