Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Yafanya Ziara ya Kikazi TCAA
Автор: Tanzania Civil Aviation Authority - TCAA TV
Загружено: 2026-02-19
Просмотров: 29
Описание:
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imefanya ziara ya kikazi katika Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa lengo la kujionea utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo, kubadilishana uzoefu, pamoja na kujadili mikakati ya kuimarisha usimamizi na maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini.
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania ni taasisi ya umma yenye jukumu la kudhibiti sekta ya usafiri wa anga katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mamlaka iliundwa kwa Sheria ya Usafiri wa Anga, Sura ya 80 (R.E 2006).
Majukumu ya kisheria ya Mamlaka ni kudhibiti masuala ya ki-usalama, ki-uchumi katika usafiri wa anga na kutoa huduma za uongozaji ndege.
Pia Mamlaka inatoa huduma za uongozaji ndege kwenye vituo vya ndege kumi na nne (14) ambavyo ni: Dar es Salaam, Kilimanjaro,Tanga, Arusha, Mwanza,Tabora,Kigoma, Dodoma, Iringa, Songwe, Songea, Mtwara, Zanzibar na Pemba
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: