🔴 BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC LAPITISHA RASIMU YA BAJETI BILIONI 34.5, 2026/27
Автор: RUVUMA TV
Загружено: 2026-02-05
Просмотров: 77
Описание:
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma limepitisha rasimu ya makadirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya shilingi bilioni 34.5, kwa ajili ya kuendesha shughuli mbalimbali za halmashauri na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Bajeti hiyo inaonesha ongezeko la asilimia 7.48 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Akiwasilisha rasimu hiyo ya bajeti kwenye kikao cha Baraza la Madiwani kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Venatus Venetus amesema kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 3.588 zinatarajiwa kukusanywa kutoka mapato ya ndani, sawa na asilimia 10.4, huku shilingi bilioni 30.927 zikitoka Serikali Kuu na wahisani, ambazo ni sawa na asilimia 89.6 ya bajeti yote..
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: