WAKAAZI WA MWACHOME WAPEWA MAFUNZO YA KIFEDHA KABLA YA KUFIDIWA NA BAMBURI
Автор: Kwale Press Club
Загружено: 2026-02-18
Просмотров: 35
Описание:
Wakazi wa Kijiji cha Mwachome eneo bunge la Matuga Kaunti ya Kwale, wameanza kupokea mafunzo ya uelewa wa kifedha kabla ya malipo ya fidia yanayotarajiwa kufanyika kwa ajili ya ununuzi wa ardhi unaolenga ujenzi wa kiwanda kipya cha kuzalisha klinka cha Bamburi Cement Plc.
Mradi wa uchimbaji wa udongo aina ya shale unatarajiwa kusaidia katika uendeshaji wa kiwanda hicho kipya.
Takribani kaya 82 zitaathirika na kuhamishwa ili kupisha mradi huo, ambao utasambaza Nzarabe (shale) kwa kiwanda kipya cha klinka.
Kwa mujibu wa Chifu Msaidizi Saidi Ali, fedha za fidia zinatarajiwa kuanza kuingia kwenye akaunti za wanufaika wiki hii.
Mafunzo hayo yanatekelezwa na Bamburi Cement kwa ushirikiano na Earth Resources Exploration Limited pamoja na Kwale Grass Root Voices, yakilenga kuwawezesha wakazi kusimamia fedha zao kwa umakini na kuepuka matumizi mabaya.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: