VIWANDA VILIVYOKUFA TANGA KUANZA UZALISHAJI JANUARI 2026
Автор: CLOUDS HABARI
Загружено: 2025-10-13
Просмотров: 71
Описание:
VIWANDA VILIVYOKUFA TANGA KUANZA UZALISHAJI JANUARI 2026
Ufufuaji wa viwanda ambavyo vilidorora kwa miaka kadhaa jijini Tanga umeanza rasmi kwa viwanda vikuu vitatu kutangazwa kuwa katika hatua za mwisho za maandalizi ya kurejea katika uzalishaji wake
Tanga, zamani ilikuwa ni Mkoa wa pili kwa viwanda baada Dar Es Salaam lakini ilikumbwa na kudorora kwa uzalishaji na kupotea kwa ajira. Leo, serikali kwa kushirikiana na wawekezaji, imeanzisha mpango wa kufufua viwanda ili kuimarisha uchumi na kurejesha ajira kwa wananchi. #cloudsdigitalupdates
Akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kutembelea viwanda vilivyokuwa vinazalisha bidhaa za chuma, bidhaa zitokanazo na misitu,katibu mkuu wizara ya viwanda na bishara Hashil Abdallah amesema mpango wa ufufuaji unatokana na uwezezeshwaji wa kisera na kimiongozo uliofanya na Rais Samia.
Hata hivyo Richard Mukama na Christopher Mzava ambao ni wafanyakazi wa Kiwanda Cha Africa Hamoni wakatumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa kuamua kufanya ufufuaji wa viwanda .
@saidraisa
#cloudsDigitalUpdate
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: