MKURUGENZI MTENDAJI NYASA AAGIZWA KUCHUKUA HATUA KWA WATUMISHI WAZEMBE
Автор: Site Tv Online
Загружено: 2025-06-18
Просмотров: 230
Описание:
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ametakiwa kuchukua hatua za kinidhamu mapema dhidi ya watumishi wote watakaosababisha hasara au hoja kutokana na uzembe kazini.
Agizo hilo limetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi Mary Makondo, wakati wa Baraza Maalum la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024.
Bi Makondo amesema licha ya Halmashauri ya Nyasa kupata hati safi katika ripoti ya CAG, bado kulikuwa na hoja 41 zilizobainishwa, ambapo 24 kati ya hizo zimeshafanyiwa kazi na kufungwa, 10 zinaendelea kufanyiwa kazi huku hoja 12 zikisalia bila utekelezaji. Amesisitiza kuwa watumishi wanaohusika na uzembe wa kusababisha hoja hizo wachukuliwe hatua kali za kinidhamu ili kuepusha kurudia makosa hayo.
Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Ndugu Oddo Mwisho, amezitaka halmashauri zote mkoani humo kuwatumia kikamilifu wakaguzi wa ndani wa hesabu za serikali. Amesema hatua hiyo itasaidia kubaini mapema dosari za kiutendaji na hivyo kupunguza hoja katika ripoti za ukaguzi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: