Kilio cha Wakulima Katavi kwa Serikali//Hakuna Skimu ya Umwagiliaji iliyokwisha kamilika.
Автор: Site Tv Online
Загружено: 2021-06-11
Просмотров: 802
Описание:
#NEWS Licha ya Serikali kuwekeza zaidi ya Bilioni 5 kwa ajili ya Skimu tatu za Umwagiliaji zilizopo Wilayani Mpanda ambazo ni Ugala,Mwamkulu na Uruila,Mkoa wa Katavi hauna Skimu iliyokamilika pamoja na kuwa Mpango wa Serikali wa Mwaka 2021/22 ni kuboresha Kilimo cha Umwagiliaji Nchini.
Hayo yanakuja mara baada ya Wakulima katika Kijiji cha Majalila Kata ya Tongwe Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi kusikiliza Hotuba aliyoitoa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Mwigulu Nchemba kuhusu Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22 katika Sekta ya Kilimo kuwa Maeneo yatakayopewa msukumo ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji.
Kwa Mkoa wa Katavi Serikali ilitenga kiasi cha shilingi Bilioni 5.6 kwa Skimu tatu za Umwagiliaji ambapo Skimu ya Ugalla ilitengewa Sh. Bilioni 1.2, Skimu ya Umwagiliaji ya Mwamkulu ilitengewa Sh. Bilioni 1.6 na Skimu ya Uruila ilitengewa Sh. Bilioni 1.8 lakini bado hazijakamilika.
#SiteNews
#TukutaneSite
#TukutaneKazini
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: