RC KUNENGE AZINDUA KIWANDA KIKUBWA CHA MAGODORO AFRIKA MASHARIKI
Автор: Habari Na Zaidi
Загружено: 2026-03-18
Просмотров: 265
Описание:
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, leo Machi 17, 2026 amezindua rasmi kiwanda kikubwa cha kutengeneza magodoro Afrika Mashariki, hatua inayozidi kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha uwekezaji na viwanda nchini.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Kunenge amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira bora na rafiki kwa wawekezaji ili kuvutia uwekezaji zaidi na kukuza uchumi.
Amesisitiza kuwa Mkoa wa Pwani una umeme wa kutosha kutoka Bwawa la Mwalimu Nyerere, huku hatua za usafirishaji wa umeme huo zikiendelea kuboreshwa.
Kwa upande wa miundombinu, amesema uwepo wa bandari, gesi asilia na reli ya kisasa (SGR) unaongeza urahisi wa usafirishaji na kufungua masoko mapana zaidi.
“Bagamoyo kuna ujenzi wa gati 38, ambapo gati 3 tayari zimeanza kujengwa. Pia kuna reli ya kisasa kutoka Bagamoyo hadi Kwala inayounganisha nchi nane, na sasa nchi ya tisa imeongezeka—hii itarahisisha upatikanaji wa masoko,” amesema Kunenge.
Aidha, amesema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, jumla ya viwanda 301 vimejengwa:
Vikubwa: 121, Vya kati: 114 na Vidogo: 66 Hivyo kufikisha jumla ya viwanda 1,688 hadi sasa.
Pwani inaendelea kuthibitisha kuwa kitovu kipya cha viwanda na biashara Afrika Mashariki!
#RC_Kunenge #Pwani #Bagamoyo #Tanzania #BongoNews #Habari #Viwanda #Uwekezaji #Maendeleo #Biashara #SGR #Bandari #NyerereDam
#TrendingNow #ViralNews #ExplorePage #FYP #ForYou #InstaNews #BreakingNews #AfricaRising #EastAfrica #BusinessNews #Economy #InvestInAfrica #MadeInAfrica #Entrepreneurship #BigMoves #OnTheRise #ViralPost
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: