TAZAMA NAMNA UMO ILIVYOFANYA TUKIO KUBWA LA HURUMA NA UPENDO DODOMA
Автор: WASHINDI MEDIA
Загружено: 2026-02-20
Просмотров: 23
Описание:
#serikali #subscribe #newsupdate #washindimediaupdates #africa #subscribemychannel #subscribenow #tanzania #dodoma #orphan #washindi #serikali
Taasisi ya Maendeleo na Uchumi (UMO) imeungana na wadau mbalimbali jijini Dodoma kutoa msaada na kuonesha matendo ya huruma kwa watoto yatima katika Kituo cha Rahman Orphanage Centre kilichopo Chang’ombe, ikiwa ni sehemu ya kuenzi mwezi mtukufu wa Ramadhani sambamba na Kwaresma.
Akizungumza leo Februari 20, 2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Mhe. Alhaj Jabir Shekimweri, mwakilishi wake Kassim Jonjolo aliipongeza UMO kwa juhudi zake za kusaidia wahitaji na kuhamasisha taasisi nyingine kuiga mfano huo.
Alisisitiza kuwa matendo ya huruma hayapaswi kufanyika wakati wa vipindi maalum vya kiimani pekee, bali yawe sehemu ya maisha ya kila siku.
“Tunapenda kuipongeza UMO kwa kazi kubwa wanayoifanya. Tunaendelea kuhamasisha taasisi nyingine kuungana nao, kwani vituo vya watoto yatima ni vingi hapa Dodoma na vinahitaji msaada wa kila mmoja wetu,” alisema Jonjolo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Rahman Orphanage Centre, Rukia Hamisi Abdallah, aliishukuru UMO kwa kuandaa tukio hilo maalum na kusaidia watoto waliopo kituoni hapo. Alieleza kuwa kituo hicho kina watoto 120, wengi wao wakipatiwa mafunzo ya kujiajiri hususan katika sekta ya kilimo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: