UNDANI: MUME KUKIRI Kumuua MKEWE na KUMCHOMA kuwa MAJIVU!
Автор: Global TV Online
Загружено: 2019-07-17
Просмотров: 312110
Описание:
UNDANI:MUME KUKIRI Kumuua MKEWE na KUMCHOMA kuwa MAJIVU!
Mume wa mwanamke anayedaiwa kupotea kwa zaidi ya miezi miwili, Naomi Marijani (36), Khamis Luwongo (Meshack), amekiri kumuua mkewe na kisha kumchoma kwa mkaa magunia mawili na kumzika shambani kwake.
Mwanamke huyo anadaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na picha yake kusambazwa katika mitandao ya kijamii sanjari na taarifa za kutoweka kwake.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kigamboni, Thobias Walelo mtuhumiwa huyo anayeshikiliwa na polisi kwa sasa, katika maelezo yake amedai mara baada ya mauaji hayo aliuchukua mwili wa mke wake na kuuweka kwenye shimo alilochimba kwenye banda lake la kufugia kuku.
Amedai baada ya kuuweka shimoni aliweka mkaa magunia mawili na mafuta ya taa kisha akawasha moto ulioteketeza mwili wote hadi kubaki majivu kisha alichukua majivu hayo akaweka kwenye mfuko na kubeba kwa kutumia gari lake lenye namba T206CEJ, Subaru Forester yenye rangi nyeusi na kuupeleka shambani kwake lililoko Kijiji cha Mlogolo, mkoani Pwani.
#MAUAJI #AMCHOMA MKEWE MOTO
https://www.youtube.com/playlist?list... https://www.youtube.com/watch?v=N1X-f... Watch More Videos here: https://goo.gl/GvVdZw Watch More Videos here: https://goo.gl/ae33fL Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook:
www.facebook.com/globalpublishers Instagram
www.instagram.com/globalpublishers Twitter: www.twitter.com/GlobalHabari Install Global App: ANDROID: https://goo.gl/QvT6RV Install Global App: iOS: https://goo.gl/2jDyho
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: