ycliper

Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
Скачать

Miembe yenye Miaka 100 inavyowatesa wakazi Morogoro, Historia yake yaanikwa

Автор: Mwananchi Digital

Загружено: 2024-11-05

Просмотров: 2215

Описание: Wakazi wa mtaa wa Boma Road, manispaa ya Morogoro, wameeleza historia ya miti ya miembe yenye zaidi ya miaka 100 iliyopandwa enzi za utawala wa Wajerumani.

Wakisimulia hadithi walizorithishwa na mababu zao, wakazi hao wamesema miembe hiyo ilipandwa kama sehemu ya uhifadhi wa mazingira na pia kama adhabu kwa watu walioonekana kukosea wakati huo.

Wajerumani walitawala Tanganyika kuanzia mwaka 1889 na kujenga maboma katika baadhi ya mikoa, ikiwemo Morogoro. Ili kupendezesha maeneo ya maboma yao, walipendelea kupanda miti kwenye barabara zinazoelekea maboma hayo.

Barabara maarufu ya Boma Road, inayoingia mpaka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, ni mojawapo ya maeneo yenye historia ya miembe hiyo.

Kwa mujibu wa Sudi Ramadhan Kiroboto, mkazi wa Boma Road, miembe hiyo imekuwa sehemu ya maisha yao kwa muda mrefu, ikiwa na faida kama kivuli, matunda, na mandhari nzuri. Kiroboto alisema,

"Tumeikuta hii miembe, na kweli imetulea, kwasababu tumekula sana matunda yake na tunapata kivuli kizuri tunapopumzika nje."

Wakazi wanaeleza kuwa, zamani, miembe hiyo ilikuwa na mavuno mengi, na matunda yake yaliwasaidia baadhi ya watu kupata kipato, Hata hivyo, kutokana na umri mkubwa wa miti hiyo, uzalishaji wa matunda umepungua, Pia, matawi ya miembe hiyo yamekuwa yakianguka mara kwa mara, hasa wakati wa mvua na upepo mkali, hali inayosababisha hasara kwa nyumba na miundombinu ya umeme.

Kiroboto anaeleza kuwa wakazi wa Boma Road wamewahi kutoa malalamiko kwa serikali kuhusu hatari inayoweza kusababishwa na miembe hiyo, na walishauriwa kupunguza matawi, lakini gharama yake ni kubwa.

Issa Mkwembo, mkazi mwingine, alisema kuwa miembe hiyo inabeba historia na inawakumbusha madhara ya ukoloni, akiiomba serikali kuipunguzia matawi mara kwa mara ili isilete madhara kwa jamii.

"Miembe hii ni historia na ni alama ya madhara ya ukoloni wa kijerumani, na vizazi vijavyo vinapaswa kujifunza kupitia mifano hii hai, hivyo, ni vyema serikali iangalie namna bora ya kuitunza na kuipunguzia matawi kila baada ya muda," alisema Mkwembo.

Mwananchi ilifika ofisi ya Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira katika manispaa ya Morogoro kujua mikakati ya serikali katika kuhakikisha miembe hiyo haitaleta madhara kwa jamii.

Dawson Jeremiah, mkuu wa kitengo hicho, alisema kuwa serikali haina mpango wa kukata miembe hiyo kwa kuwa ina thamani ya kihistoria na pia inapendezesha barabara hiyo maarufu ya Boma Road.

"Kwanza kabisa, hatuna mpango wa kukata hii miembe, licha ya kuwa ni historia lakini pia inapendezesha barabara yetu inayoanzia stendi ya zamani ya Hice mpaka ofisi za Mkuu wa Mkoa," alisema Jeremiah.

Aliongeza kuwa miti hiyo ina uwezo wa kuishi kwa muda mrefu kutokana na aina ya mbegu zilizopandwa enzi za Wajerumani, ambazo zinahimili mazingira na kuishi kwa muda mrefu.

Alitoa wito kwa wakazi wa eneo hilo kuacha kulundika takataka kwenye mashina ya miembe na kuzichoma moto kwani tabia hiyo inadhoofisha miti na kuifanya ianguke.

"Kwa kushirikiana na ofisi ya kata, tuna taratibu za kushughulikia matawi yanayoonyesha dalili za kuanguka kwa kutoa taarifa na kuyashughulikia mara moja," alieleza Jeremiah.

Не удается загрузить Youtube-плеер. Проверьте блокировку Youtube в вашей сети.
Повторяем попытку...
Miembe yenye Miaka 100 inavyowatesa wakazi Morogoro, Historia yake yaanikwa

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио

Похожие видео

MJUE CHIEF KINGALU MWANABANZI ANAYEISHI ZAIDI YA MIAKA 400 SASA

MJUE CHIEF KINGALU MWANABANZI ANAYEISHI ZAIDI YA MIAKA 400 SASA

EXCLUSIVE: UKWELI KUHUSU DARAJA LA MITI LA MILIONI 31 MOROGORO

EXCLUSIVE: UKWELI KUHUSU DARAJA LA MITI LA MILIONI 31 MOROGORO

“KILAKALA” - A Village Within the City of Morogoro | Tanzania is Blessed 2024 | 4K Quality

“KILAKALA” - A Village Within the City of Morogoro | Tanzania is Blessed 2024 | 4K Quality

DIWANI MOROGORO ASIMAMISHWA KAZI KISA MITANDAO

DIWANI MOROGORO ASIMAMISHWA KAZI KISA MITANDAO

ZIMEFICHUKA SABABU WALIOCHOMA GARI MSIBANI MOROGORO/KUNA MAZINGAOMBWE CHANZO CHA KIFO CHA MAREHEMU

ZIMEFICHUKA SABABU WALIOCHOMA GARI MSIBANI MOROGORO/KUNA MAZINGAOMBWE CHANZO CHA KIFO CHA MAREHEMU

Unafahami historia ya jina la Matombo?

Unafahami historia ya jina la Matombo?

AJALI: DEREVA BODABODA AGONGWA NA LORI MOROGORO, MASHUHUDA WASIMULIA, PIKIPIKI ILITELEZA

AJALI: DEREVA BODABODA AGONGWA NA LORI MOROGORO, MASHUHUDA WASIMULIA, PIKIPIKI ILITELEZA

LIVE: MAGUFULI AKIZINDUA  SOKO KUU LA MANISPAA YA MOROGORO

LIVE: MAGUFULI AKIZINDUA SOKO KUU LA MANISPAA YA MOROGORO

Morogoro:Wanawake wa Vijijini Wakabiliana na Athari za Mabadiliko Ya Tabianchi.

Morogoro:Wanawake wa Vijijini Wakabiliana na Athari za Mabadiliko Ya Tabianchi.

MAAJABU YA CHIFU KINGALU ALIYETAJWA NA RAIS MAGUFULI

MAAJABU YA CHIFU KINGALU ALIYETAJWA NA RAIS MAGUFULI "HANA KABURI, HAFI NA HATOKUFA HADI KIAMA”

LIVE: Clouds 360 na Maji Mwa Mwa Mwaa Ndani ya Morogoro I MORUWASA 🔥🔥

LIVE: Clouds 360 na Maji Mwa Mwa Mwaa Ndani ya Morogoro I MORUWASA 🔥🔥

SIMANZI! MLINZI AUWAWA KIKATILI AKIWA LINDONI MOROGORO, MZEE WA MIAKA 56

SIMANZI! MLINZI AUWAWA KIKATILI AKIWA LINDONI MOROGORO, MZEE WA MIAKA 56

MKE WA PROFESA NGOWI: “WAZIRI MWIGULU MADELU SACCOS YA MZUMBE UNIVERSITY HAWATAKI KUNIPA PESA YANGU”

MKE WA PROFESA NGOWI: “WAZIRI MWIGULU MADELU SACCOS YA MZUMBE UNIVERSITY HAWATAKI KUNIPA PESA YANGU”

FOLENI YA MAGARI BAADA YA MTO KUJAA MAJI DUMILA-MOROGORO

FOLENI YA MAGARI BAADA YA MTO KUJAA MAJI DUMILA-MOROGORO

ALICHOKIFANYA THABO MBEKI KATIKA MAKABURI WAPIGANIA UHURU

ALICHOKIFANYA THABO MBEKI KATIKA MAKABURI WAPIGANIA UHURU

GWAJIMA ''YAMEKUPATA KWASABABU NILIKATAA UTEKAJI'' GWAJIMA APIGILIA MSUMARI SAKATA LA UTEKAJI

GWAJIMA ''YAMEKUPATA KWASABABU NILIKATAA UTEKAJI'' GWAJIMA APIGILIA MSUMARI SAKATA LA UTEKAJI

PART 1: MAAJABU YA CHIEF KINGALU - MKE WAKE ALIKUFA KWA KUKIUKA MASHARTI, UKIINGIA LAZIMA UVUE SHATI

PART 1: MAAJABU YA CHIEF KINGALU - MKE WAKE ALIKUFA KWA KUKIUKA MASHARTI, UKIINGIA LAZIMA UVUE SHATI

💥 УЖАС! Удар баллистикой РФ по многолюдному центру Харькова

💥 УЖАС! Удар баллистикой РФ по многолюдному центру Харькова

Rais Magufuli Alivyokagua Ujenzi wa Daraja la Mto Kiyegeya, Kilosa Mkoani Morogoro

Rais Magufuli Alivyokagua Ujenzi wa Daraja la Mto Kiyegeya, Kilosa Mkoani Morogoro

Понты «идиотов» из Баку, Россия поддержит Армению, Алиев доулыбался

Понты «идиотов» из Баку, Россия поддержит Армению, Алиев доулыбался

© 2025 ycliper. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]