RC MRINDOKO AKABIDHI OFISI YA MACHINGA NA MAAFISA USAFIRISHAJI.
Автор: KATAVI RS
Загружено: 2025-10-27
Просмотров: 262
Описание:
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amekabidhi jengo jipya la Ofisi ya Machinga na Maafisa Usafirishaji lenye thamani ya shilingi milioni 26, ambalo linatarajiwa kuhudumia wafanyabiashara wadogowadogo zaidi ya 12,000 kutoka ndani ya Mkoa wa Katavi.
Makabidhiano na uzinduzi wa jengo hilo yamefanyika leo, Oktoba 27, 2025, mjini Mpanda, ambapo sambamba na kukabidhi samani na vifaa vya ofisi hiyo, RC Mrindoko amewataka wajasiriamali wa mkoa huo kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na serikali.
“Jumla ya shilingi bilioni 9 zimetolewa na serikali katika halmashauri za Mkoa wa Katavi ili kuwezesha uendeshaji wa shughuli za kiuchumi kwa wajasiriamali kupitia makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Nawaomba makundi haya yaendelee kuthamini mikopo hii na kuitumia ipasavyo,” alisema RC Mrindoko.
Awali, Katibu Tawala Msaidizi upande wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Florence Chrisant, akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, alisema serikali inaendelea kubaini makundi mbalimbali ya kijamii na kuyawezesha ili yajenge uwezo wa kiuchumi.
Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mratibu wa Machinga wa Manispaa ya Mpanda, Bw. Maiko Shabani, alisema kuwa kuwaleta pamoja wafanyabiashara wadogowadogo kutaimarisha ushirikiano kati ya makundi hayo na kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii.
Kwa upande wao, viongozi wa makundi hayo wameishukuru serikali kwa kuboresha miundombinu, kuwaratibu, kuwasimamia, pamoja na kuwawezesha kupata mitaji ya kuendesha biashara zao kupitia mikopo ya wamachinga inayotolewa na taasisi za kifedha na halmashauri.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: