RC MRINDOKO AAGIZA HATUA KALI KUFUATIA UCHELEWAJI WA MRADI WA DARAJA LA MIRUMBA.
Автор: KATAVI RS
Загружено: 2025-11-11
Просмотров: 445
Описание:
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mirumba katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.
RC Mrindoko amesema kuwa daraja hilo ni muhimu kwa wananchi kwani litaondoa tatizo la mafuriko na kurahisisha usafiri wa mazao kwenda mkoa jirani wa Rukwa. Hata hivyo, ameonesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi, akimtaja mkandarasi M/s Safari General Business Co. Ltd kwa kuchelewa kukamilisha kazi.
Ameagiza mkandarasi kuwepo saa 24 kwenye eneo la mradi, huku kazi zikiendelea usiku na mchana, na amempa masaa 72 kuhakikisha vifaa vyote muhimu vimewasili. Aidha, RC Mrindoko amempa mkandarasi wiki mbili kuonyesha maendeleo, na akisisitiza kuwa hatua kali za kimkataba zitatumika endapo ndani ya muda huo hakuna mabadiliko yoyote.
Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Katavi, Mhandisi Martin Mwakabende, amesema mradi unahusisha ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 60 katika barabara ya Katete – Kibaoni. Daraja jipya la aina ya Bailey litaimarisha usafiri wa watu na mizigo, tofauti na daraja lililokuwepo lililokuwa na uwezo mdogo wa kuhimili magari makubwa, hasa mvua.
Mradi unafadhiliwa na International Development Association (IDA) kwa gharama ya shilingi bilioni 6.39 (bila VAT), ukitekelezwa na M/s Safari General Business Co. Ltd kwa ushirikiano na Mbuya’s Co. Ltd, chini ya usimamizi wa TANROADS – TECU.
Mkataba wa mradi ni wa miezi 12, kuanzia 27 Novemba 2024 hadi 27 Novemba 2025, na hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 38, ikilinganishwa na muda uliotumika asilimia 91.6, jambo linaloonyesha kuwa kasi ya ujenzi bado ni ndogo.
Mhandisi Mwakabende amesisitiza kuwa TANROADS itaendelea kufuatilia mradi ili uhakikishe unakamilika kwa ubora na kwa wakati uliopangwa, na kwamba ujenzi wa Daraja la Mirumba ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuboresha barabara, kuimarisha uchumi wa wananchi na maendeleo endelevu katika Mkoa wa Katavi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: