UCHANGANUZI | TRA yaimarisha ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa kisasa wa IDRAS
Автор: UTV Tanzania
Загружено: 2026-02-25
Просмотров: 176
Описание:
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema maboresho ya mfumo wa kielektroniki wa usimamizi wa kodi, IDRAS, yamechangia kuongezeka kwa idadi ya walipa kodi nchini.
Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Afisa Mkuu wa Usimamizi wa Kodi wa TRA, Buluba Kanuda, amesema ongezeko hilo limetokana na ushirikishwaji mkubwa wa wananchi katika kulipa kodi pamoja na maboresho ya utaratibu wa makato ya kodi kwa waajiriwa.
Ameeleza kuwa tofauti na ilivyokuwa awali ambapo baadhi ya waajiriwa walitegemea waajiri wao kushughulikia kikamilifu masuala ya kodi, mfumo wa sasa unamwezesha mwajiriwa kufuatilia na kuthibitisha malipo yake moja kwa moja, jambo lililoongeza uwajibikaji na uwazi.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: