MTINDIO WA UBONGO: Sababu, Dalili, Matibabu
Автор: WikiElimu
Загружено: 2026-03-03
Просмотров: 26
Описание:
Katika video hii inazungumza kuhusu sababu, dalili, matibabu, namna ya kuzuia, matarajio baada ya matibabu ya MTINDIO WA UBONGO , endelea angalia mpaka mwisho kujifunza
Mtindio wa ubongo (cerebral palsy), ni hali inayosababishwa na matatizo ya ubongo ambayo yanayopelekea kuvurugika kwa shughuli za mfumo wa neva. Shughuli kama kujongea, kutembea, kujifunza, kusikia, kuona na kufikiri.
Neno utindio wa ubongo linatumika kuwakilisha matatizo yote ya mfumo wa fahamu yanayotokea utotoni na yanayothiri mjongeo na misuli ya mtoto.
Hali ya mtoto mwenye mtindio wa ubongo haibadiliki – kama alikuwa na matatizo ya kuona, hategewei kwamba ataanza kuona baada ya muda. Mtindio wa ubongo kwa watoto unaathiri zaidi misuli.
Tatizo la mtindio wa ubongo linasababishwa na matatizo kwenye maeneo ya ubongo yanayodhibiti mjongeo wa mwili. Ugonjwa wa mtindio wa ubongo unaweza kusababisha misuli inakaza au inalegea.
Sababu za mtindio wa ubongo?
Tatizo la mtindio wa ubongo linaweza kusababishwa na kuharibika kwa ubongo baada ya kukosa oksijeni kwa muda. Watoto wanaozaliwa wakiwa njiti – hawa ni wale watoto wanaowahi kuzaliwa kabla ya wiki 37 za ujauzito kukamilika – wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata mtindio wa ubongo
Mtindio wa ubongo unaweza pia kutokea utotoni kwa sababu mbalimbaliz, kama:
• Kuvuja damu ndani ya ubongo
• Majeraha ya kichwa
• Maambukizi kwenye ubongo
• Maambukizi kwa mama wakati wa ujauzito
Lakini, kuna baadhi ya visa vya mtindio wa ubongo ambavyo sababu haijulikani kabisa.
Je, nini dalili za mtindio wa ubongo?
Dalili za wagonjwa wenye mtindio wa ubongo zinatofautiana, kuna mbao wana dalili za kadri au kali sana – dalili zinaweza kuwa upande mmoja au pande zote mbili - zinaweza kuwa kwenye mikono, miguu au mikono na miguu kwa pamoja.
Kuna baadhi ya wagonjwa misuli inakaza inakuwa ngumu kuinyoosha. Kadri muda unavyokwenda misuli inaendelea kukaza zaidi.
• Misuli inakaza na inakuwa ngumu kuinyoosha. Misuli inaweza kuendelea kukaza zaidi kadri muda unavyokwenda. Kwa sababu ya kukaza kwa misuli inakuwa ngumu kutembea – magoti yakuwa nayagusana au kuvukana au unakuta mtu anatembelea vidole vya miguu na wakati mwingine viungo vinakuwa vigumu
Wagonjwa wengine:
• Wanatetemeka
• Wanatembea wakiwa wanayumbayumba
• Misuli inakuwa inalegea, hasa wakati wa mapumziko.
Dalili nyingine za mtindio wa ubongo ni:
• Kupungua kwa uwezo wa kujifunza na kufikiri, lakini wakati mwingine uwezo wa kufikiri unaweza kuwa sawa.
• Matatizo ya kuongea
• Matatizo ya kusikia au kuongea
• Maumivu, hasa kwa watu wazima (inaweza kuwa vigumu kuyadhibiti)
• Matatizo wakati wa kula
• Kushindwa kunyonya au kula kwa watoto wachanga, au kushindwa kutafuna na kumeza kwa watoto wakubwa na watu wazima
• Matatizo ya kumeza chakula (kwa rika zote)
• Kutapika na kufunga choo
Dalili nyingine ni
• Kutokwa na mate
• Kupumua kusiko kwa kawaida
• Kujikojolea
Utambuzi wa mtindio wa ubongo
Kwa mgonjwa wa mtindio wa ubongo, uchunguzi wa neurolojia ni muhimu. Kwa wazee, kupima uwezo wa kujitambua ni muhimu. Lakini pia, daktari anaweza kupima vipimo vya damu, CT scan, EEG, MRI na vipimo vya macho
Uchaguzi wa matibabu ya mtindio wa ubongo
• Mtindio wa ubongo hauwezi kuponywa, lakini matibabu mara nyingi yanaboresha uwezo wa mtoto. Watoto wengi wanaweza kuishi maisha angalau kama kawaida wanapokuwa watu wazima kama watapata matibabu sahihi. Kwa kawaida, kadiri matibabu yanavyowahi kutolewa ndivyo na matokeo yanavyoboreka.
• Matibabu yanajumuisha mazoezi, kujifunza kazi, kujifunza kuongea, madawa kudhibiti degedege, madawa kulegeza misuli iliyokakamaa, madawa ya maumivu, upasuaji kuondoa kasoro zilizopo, viatu maalumu, kiti cha magurudumu na vifaa vya mawasiliano kama kompyuta n.k.
• Lengo la matibabu ni kumsaidia mtu kujitegemea kwa kadri inavyowezekana. Matibabu yanahitaji ushirikiano wa wataalamu wa fani mbalimbali - Madaktari wa kawaida, madaktari wa meno (wanapaswa kuangaliwa meno kila baada ya miezi 6), watu wa utawi wa jamii, wauguzi, wataalamu wa kufundisha kazi, wataalamu wa mazoezi, wataalamu wa kufundisha kuongea, madaktari bingwa wa mfumo wa neva, madaktari bingwa wa
Emmanuel Mniko #mniko #wikielimu @wikielimu
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: