WLAC yawasaidia wanawake waathirika wa ukatili nchini Tanzania
Автор: Habari za UN
Загружено: 2026-03-05
Просмотров: 41
Описание:
#HabarizaUN #UmojawaMataifa #Kiswahili #UNNewsKiswahili #wilac #Tanzania #Kagera
Kuelekea Siku ya wanawake Duniani itakayoadhimishwa tarehe 8 Machi, mwaka huu ikijikita na haki, na haki ya kisheria kwa wanawake, tunakupele nchini Tanzania kumsikia mmoja wa wanawake wanufaika na msaada kutoka Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake WLAC, aliyekuwa akinyanyaswa na mumewe na kufukuzwa bila chochote.
Katika kijiji cha Ijumbi, wilayani Muleba Mkoani Kagera Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, hii ni simulizi ya Ansfrida Prospeli ambaye ni sauti ya maumivu, lakini pia ya ushindi. Kwani kwa miaka kadhaa aliishi ndani ya ndoa yenye ukatili, kipigo, kufukuzwa usiku, na hata kupelekwa hospitalini baada ya kupoteza fahamu kutokana na kipigo. Leo, anasimama imara, akisema haki inawezekana.
Pata taarifa ya habari, makala, habari kwa picha , mahojiano na matukio kuhusu masuala ya kibinadamu, SDGs na mengine mengi kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa. Ni "Habari za UN" kutoka makao makuu ya UN New York City.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: