KESI YA WAGOMBEA WA ACT PEMBA YAAHIRISHWA HADI DESEMBA 23
Автор: Nipashe Digital
Загружено: 2025-12-16
Просмотров: 732
Описание:
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Kanda ya Pemba, Chausiku Kuya, ameahirisha kesi ya madai iliyofunguliwa na waliokuwa wagombea wanane wa Uwakilishi kupitia chama cha ACT Wazalendo Kisiwani Pemba hadi Desemba 23, 2025.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya mawakili wa upande wa wadai kuiomba Mahakama iwape muda wa siku saba ili kupitia majibu ya maandishi yaliyowasilishwa na upande wa utetezi, pamoja na kuandaa majibu ya kinzani kwa kina na kwa kuzingatia taratibu za kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Mwanasheria Mkuu wa ACT Wazalendo, Wakili Omar Said Shaaban, ambaye pia ni kiongozi wa jopo la mawakili wa wadai, alisema kuwa ombi la kupewa muda lililenga kuhakikisha hoja zote za utetezi zinajibiwa kwa usahihi na kwa kufuata misingi ya sheria.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: