Familia moja katika kijiji cha Kusumek eneobunge la Bureti inataka uchunguzi wa mauwaji ya mtoto wao
Автор: Citizen TV Kenya
Загружено: 2026-02-12
Просмотров: 244
Описание:
Familia moja katika kijiji cha Kusumek eneobunge la Bureti inadai haki kufuatia kifo cha mwana wao katika mazingira yasiyoeleweka.
Kwa mujibu wa waliokuwa wakiishi naye, Brian alipokea simu majira ya saa tisa asubuhi ya kuamkia Jumanne, na kisha akaondoka nyumbani na hakurejea tena. Baadaye, mwili wake ulipatikana kando ya barabara. Familia hiyo imepinga ripoti ya polisi iliyoeleza kuwa Brian alifariki kutokana na ajali. Polisi wanasema aligongwa na gari lililokuwa likienda kwa kasi , ilhali familia inasema kuwa majeraha aliyokuwa nayo kwenye mwili wake yanaonyesha kuwa aliuawa. Simu ya marehemu ambayo ilikuwa imepotea lakini baadaye kupatikana, huku polisi wakisema uchunguzi kuhusu kilichotokea bado unaendelea. Brian alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho wa taasisi ya kiufundi ya Belgut .
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: