Lowassa Afunguka Alivyohojiwa na DCI, Aachiwa kwa Dhamana
Автор: Global TV Online
Загружено: 2017-06-27
Просмотров: 84019
Описание:
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa amefunguka kuhusu alivyohojiwa kwa saa nne katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ambapo baada ya kuhojiwa ameachiwa kwa dhamana na kuondoka makao makuu ya polisi majira ya saa 8.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuachiwa, Lowassa alisema aliitwa na polisi kutokana na hotuba yake aliyoitoa siku chache zilizopita, nyumbani kwa mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara kuhusu suala la mashehe wa uamsho wanaoshikiliwa kwa zaidi ya miaka minne sasa.
Lowassa alisema anawaomba wafuasi wake wote watulie na kuongeza kwamba ameambiwa arejee tena kwa mahojiano Alhamisi ya wiki hii.
Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Vincent Mashinji, alisema kuwashikilia wafuasi wa uamsho kwa kipindi chote hicho, bila kupandishwa mahakamani ni makosa na ni kinyume na haki za binadamu. Akawaomba wafuasi wa Chadema na wapenda maendeleo, watulie katika kipindi hiki.
Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe / uwazi1
Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya…
/ uwazi1
/ uwazi1
/ uwazi1
WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/
FACEBOOK: / globalpublishers
TWITTER: / globalhabari
INSTAGRAM: / globalpublishers
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: