ycliper

Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
Скачать

TUME YA MADINI TV

Автор: Tume ya Madini

Загружено: 2026-01-27

Просмотров: 45

Описание: MAPINDUZI MAKUBWA UWEZESHAJI MITAJI KWA WACHIMBAJI WADOGO

▪️Wizara ya Madini na CRDB waingia makubaliano ya utekelezaji wa programu

▪️Wachimbaji wadogo kukopeshwa Mitambo ya Uchenjuaji (CIP), Vifaa vya Kuchimba na Fedha za Uendeshaji

▪️Kikundi cha SAZA GOLD FAMILY wakaribia kuanza kunufaika kupitia leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na BAFEX

▪️Ni leseni aliyoelekeza Rais Samia kwa wachimbaji wadogo


Dodoma

Ikiwa ni mkakati wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kimitaji, Wizara ya Madini imeingia makubaliano na Benki ya CRDB kupitia programu maalum kwa ajili ya kuwasadia wachimbaji wadogo kwa kuwapatia mikopo kwa ajili ya ununuzi wa mitambo ya uchenjuaji (CIP), vifaa na gharama za uendeshaji.

Akizungumza kwenye kikao cha kujadili mapendekezo ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini katika utoaji wa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini, Waziri Mavunde amesema kupitia makubaliano haya, wachimbaji wadogo wenye leseni za madini wataweza kuomba na kupatiwa mikopo na benki hiyo na kuwezesha uzalishaji wao kuwa wenye tija na mchango wao kuendelea kukua kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali.


Akielezea moja ya wanufaika wa programu hiyo Waziri Mavunde amesema kuwa ni pamoja na kikundi cha SAZA GOLD FAMILY ambapo Benki ya CRDB ipo mbioni kutoa mkopo wa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ununuzi wa mtambo wa kuchenjua madini ya dhahabu na vifaa vya uchimbaji kwa kikundi hicho kinachoendesha shughuli zake katika eneo la Saza mkoani Songwe.

Ameendelea kusema kuwa awali, kupitia ziara ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu katika eneo la Saza, kikundi cha wachimbaji wadogo kupitia Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mulugo waliomba kupatiwa leseni ya uchimbaji wa madini, ambapo Rais Samia alielekeza kikundi hicho kupatiwa leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na Kampuni ya BAFEX.

Amesema ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kikundi cha SAZA GOLD FAMILY kilipewa leseni na kuanza kuchimba madini na kuomba mkopo kwa ajili ya mtambo wa uchenjuaji wa madini na vifaa ambapo mchakato wake ulianza mara moja kupitia Benki ya CRDB.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ameitaka Tume ya Madini na Benki ya CRDB kukamilisha Makubaliano ya Awali (MoU) ifikapo Jumatano ijayo ili taratibu za utoaji wa mkopo zikamilike mapema.

Ameeleza manufaa ya mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini kuwa ni pamoja na uzalishaji kuongezeka na mchango wao kuongezeka kwenye ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali hasa ikizingatiwa kwa sasa wanachangia asilimia 40.

Wakati huohuo, Mhe. Mavunde amezitaka Taasisi za Fedha nchini kuwaamini wachimbaji wadogo wa madini kwa kuweka mazingira rafiki ya mikopo kwani wana utajiri mkubwa wa rasilimali za madini.

“Ninaomba Taasisi za Fedha kuwaamini wachimbaji wa madini kwa kuwa wenyewe kwa wenyewe wana uwezo wa kukopeshana hadi shilingi bilioni tano kwa kuaminiana, mkiweka mazingira mazuri na kuwakopesha mtapata faida kubwa sana kupitia Sekta ya Madini na kukuza mitaji yenu,” amesisitiza Waziri Mavunde.

Naye Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mlugo akizungumza kwenye kikao hicho amempongeza Waziri Mavunde kwa kuwa mlezi wa wachimbaji wadogo wa madini nchini sambamba na kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa lengo la kuhakikisha wanatajirika kupitia Sekta ya Madini.

“Ninampongeza sana Waziri Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kuwapambania wachimbaji wadogo wa madini kuanzia kwenye upatikanaji wa leseni za madini, kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa ajili ya upatikanaji wa mikopo na kutatua changamoto mbalimbali,” amesema Mulugo.

Katika hatua nyingine ameitaka Benki ya CRDB kuajiri wataalam wa madini ili kuwa na uelewa wa Sekta ya Madini hali itakayowawezesha kutoa mikopo kwa urahisi zaidi na kuweka mazingira mazuri ya ukopeshaji.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa sambamba na kupongeza Benki ya CRDB kwa nia yake ya kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini amewataka kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini kuhusu masuala ya fedha ili waweze kukopa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba ameshauri Benki ya CRDB kuendelea kuweka mazingira mazuri ya utoaji wa mikopo kwa kuangalia historia ya uzalishaji kwa wachimbaji wadogo wa madini ili waweze kukopesheka.

Wakati huohuo akizungumza kwenye kikao hicho, Mwenyekiti wa Songwe Gold Family, Simon Ndaki ameshukuru sana kwa msaada wa Serikali kwa kuwaunganisha na Benki ya CRDB na kufanikisha hatua za awali za maombi ya mkopo huo.

“Tunamshukuru sana Waziri wa Madini na timu yake kwa kutupatia leseni ya madini na kusimamia kikamilifu hatua zote za awali za maombi ya mkopo kwenye kikundi chetu chenye wanachama 264, tunaamini kupitia uzalishaji wetu kwa kutumia vifaa vya kisasa mchango wetu unakwenda kuwa mkubwa kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali,” amesema Ndaki.

Не удается загрузить Youtube-плеер. Проверьте блокировку Youtube в вашей сети.
Повторяем попытку...
TUME YA MADINI TV

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио

Похожие видео

Защита диссертации на соискание степени докт. PhD по спец. 6D030100 «Юриспруденция» Темиргазина Р.Х.

Защита диссертации на соискание степени докт. PhD по спец. 6D030100 «Юриспруденция» Темиргазина Р.Х.

Это заставляет зубы снова расти без имплантов, учёные из Японии сделали это открытие

Это заставляет зубы снова расти без имплантов, учёные из Японии сделали это открытие

Мултифондове for dummies

Мултифондове for dummies

TESLA УНИЧТОЖАЕТ РЫНОК — дом за 7 999 долларов разворачивается за часы и меняет всё!

TESLA УНИЧТОЖАЕТ РЫНОК — дом за 7 999 долларов разворачивается за часы и меняет всё!

Самоуправление: лидерский навык, который HR-специалисты не могут игнорировать | Honest HR

Самоуправление: лидерский навык, который HR-специалисты не могут игнорировать | Honest HR

TUME YA MADINI

TUME YA MADINI

Siri ya UTAJIRI kupitia SACCOS: USIKOPE kabla ya kutazama video hii!

Siri ya UTAJIRI kupitia SACCOS: USIKOPE kabla ya kutazama video hii!

⚡️Трамп СОРВАЛСЯ УЛЬТИМАТУМОМ к Зеленскому! У Путина НАЕХАЛИ на США! Китай ВСТУПИЛ В ВОЙНУ. ЭПШТЕЙН

⚡️Трамп СОРВАЛСЯ УЛЬТИМАТУМОМ к Зеленскому! У Путина НАЕХАЛИ на США! Китай ВСТУПИЛ В ВОЙНУ. ЭПШТЕЙН

Жириновский: остатки Ирана и Турции войдут в состав России! Воскресный вечер с Соловьевым. 13.05.18

Жириновский: остатки Ирана и Турции войдут в состав России! Воскресный вечер с Соловьевым. 13.05.18

ЛИПСИЦ: КАТАСТРОФА ПРИШЛА В МОСКВУ! Миллионеры РФ ТЕРЯЮТ АКТИВЫ. Цена на нефть ДАЛА ОБРАТНЫЙ ЭФФЕКТ

ЛИПСИЦ: КАТАСТРОФА ПРИШЛА В МОСКВУ! Миллионеры РФ ТЕРЯЮТ АКТИВЫ. Цена на нефть ДАЛА ОБРАТНЫЙ ЭФФЕКТ

SERIKALI YAIMARISHA ELIMU YA USHINDANI WA SOKO KWA WADAU DAR ES SALAAM

SERIKALI YAIMARISHA ELIMU YA USHINDANI WA SOKO KWA WADAU DAR ES SALAAM

Unbelievable Workers | Working with Talented Engineers #10

Unbelievable Workers | Working with Talented Engineers #10

Mwanachama Chama cha Ushirika wa Wafugaji Kiluvya (CHAWAKIM)

Mwanachama Chama cha Ushirika wa Wafugaji Kiluvya (CHAWAKIM)

TUME YA MADINI TV

TUME YA MADINI TV

САЛЫК КЫЗМАТЫ ТАШИЕВДЕН КОРКУП,  АНЫН ИШКАНАЛАРЫН ТЕКШЕРБЕЙ КЕЛГЕН

САЛЫК КЫЗМАТЫ ТАШИЕВДЕН КОРКУП, АНЫН ИШКАНАЛАРЫН ТЕКШЕРБЕЙ КЕЛГЕН

Old Bags, Big Tomatoes: A Tomato Growing Trick That Will Surprise Everyone.

Old Bags, Big Tomatoes: A Tomato Growing Trick That Will Surprise Everyone.

YANGA : VIONGOZI KULIMALIZA HILI MAPEMA MNOO? BADO HAWAJACHELEWA?

YANGA : VIONGOZI KULIMALIZA HILI MAPEMA MNOO? BADO HAWAJACHELEWA?

Правда о принцессе Дубая, которую скрывают целые страны…

Правда о принцессе Дубая, которую скрывают целые страны…

MAKONDA: BARABARA YA NJIA NANE MOSHI–ARUSHA KUFUNGUA UCHUMI WA KANDA YA KASKAZINI

MAKONDA: BARABARA YA NJIA NANE MOSHI–ARUSHA KUFUNGUA UCHUMI WA KANDA YA KASKAZINI

Вольф Мессинг о 2026 годе: архивная запись, которая всплыла спустя 53 года

Вольф Мессинг о 2026 годе: архивная запись, которая всплыла спустя 53 года

© 2025 ycliper. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]