KARANDINGA LA POLISI KUBEBA MAKADA WA CCM, RPC SIMIYU AELEZA SABABU
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2025-03-23
Просмотров: 6690
Описание:
Wakati kitendo cha karandinga ya Jeshi la Polisi kubeba makada na wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi kikiibua mjadala kwenye mitandao ya kijamii, Kamanda wa Polisi mkoani humo ametaja sababu ya makada hao kubebwa na gari hiyo.
Gari hilo lenye namba za usajili PT 4342 lilionekana limetumika kubeba wanachama hao ambao walihuduria sherehe za mkoa huo za miaka 4 ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan zilizofanyika Machi 22,2025 katika viwanja wa CCM mjini Bariadi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumapili Machi 23,2025 kwa Umma na Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu,Edith Swebe imeeleza kuwa gari hilo lilitoa msaada kwa wanachama hao walioharibikiwa na gari wakiwa njiani kuelekea mjini Bariadi.
Taarifa hiyo imezidi kueleza kuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(OC CID)wa wilaya ya Itilima ambaye alikuwa katika gari hilo la polisi alimuamuru dereva wa gari kusimamisha ili kujua wananchi hao walikuwa na tatizo gani.
Wananchi hao walieleza kuwa walikuwa wameharibikiwa na gari walikuwa wakisafiria na wakaomba msaada wa usafiri kwenye gari hilo la polisi.
Jeshi la polisi mkoa wa Simiyu linakanusha kuwa halikubeba wanachama wa CCM bali lilitekeleza wajibu wake wa kisheria wa kulinda usalama wa raia na mali zao.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: