MAGOLI: NKANA FC 2-1 SIMBA SC (CAF CL - 15/12/2018)
Автор: Azam TV
Загружено: 2018-12-15
Просмотров: 134654
Описание:
Wekundu wa Msimbazi Simba SC wamepoteza mchezo wao wa kwanza wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAF CL) kwa kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mashetani Wekundu wa Nkana FC katika mchezo uliopigwa mjini Kitwe nchini Zambia.
Simba ilionekana kuelemewa zaidi kipindi cha kwanza cha mchezo na kuruhusu bao la kwanza lilifungwa na Ronald Kampamba dakika ya 27 baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Hassan Kessy.
Kipindi cha pili Simba walionekana kuimarika na kukianza kwa kusukuma mashambulizi langoni kwa Nkana lakini walijikuta wakifanya makosa katika safu yao ya ulinzi na kuruhusu bao la pili, lililotiwa kimiani na Kelvin Kampamba dakika ya 56.
Simba walipata bao lao pekee dakika ya 73 kwa mkwaju wa penati uliofungwa na Nahodha wao John Bocco baada ya Meddie Kegere kuangushwa ndani ya eneo la hatari.
Kwa matokeo hayo sasa Simba itahitaji ushindi wa kuanzia bao 1-0 katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Jijini Dar es Salaam, wiki moja ijayo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: