Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob Mkunda, Aridhishwa na Kasi ya Ujenzi Nyumba 5000 za Makazi Msomera
Автор: Ulinzi Channel
Загружено: 2024-01-20
Просмотров: 23609
Описание:
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa nyumba 5000 za makazi ya wananchi wanaohama kwa hiari yao kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kuja Msomea Handenj Tanga. Mradi huo unatekelezwa na Jeshi la Kujenga Taifa(JKT)
Akikagua mradi huo, Jenerali Mkunda amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo n namna Vijana wa JKT wanavyoutekeleza mradi huo kwa weledi mkubwa.
Aidha ametoa rai kwa watendaji wote katika Mradi huo kuendelea kutekeleza mradi huo kwa uzalendo mkubwa ili uweze kukidhi na kufikia matarajio ya Serikali.
Vile vile, Mkuu wa Majeshi amewapongeza vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa na amewataka kuendeleza morali ya kufanya kazi kwani huo ndio moyo wa kizalendo kwa Taifa lao.
#jwtz #jkt
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: