MAISHA NA AFYA: Kujifungua kwa upasuaji na matatizo yake.
Автор: VOA Swahili
Загружено: 2022-09-09
Просмотров: 8119
Описание:
Watoa huduma za afya hufanya upasuaji wa C-SECTION kutokana na sababu kadhaa, ikiwemo pale mama anaposhindwa kujifungua kwa njia ya kawaida na hivyo kusababisha afya ya mama au mtoto kuwa hatarini. Kesi kama hizi mara nyingi hujumuisha uchungu mkali kwa mama, mapigo ya moyo kuwa juu na matatizo mengine ya kitovu cha mtoto kujifunga.
Hata hivyo wakati mwingine C-SECTION hufanywa bila kuwepo sababu za kiafya, nikimaanisha kwamba kutokana na ombi la mama mjamzito. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO) upasuaji wa C-SECTION unaendelea kuongezeka duniani, na kwa sasa unahusisha Zaidi ya mtoto mmoja kati ya watano wanaozaliwa.
Wataalamu wanasema fursa za utaratibu salama wa C-SECTION katika jamii zilizo na mfumo duni wa afya kama vile barani Afrika ni njia bora ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito. Hata hivyo wanawake wengi hufariki kutokana na kukosa fursa ya kupata huduma bora wakati wa kujifungua, kuvuja damu kwa wingi au makossa yanayotokea wakati wa kujifungua.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: