SERIKALI YASHAURIWA KUANDAA MPANGO WA KUPANDA MITI KATA KWA KATA
Автор: DODOMA RS TV CHANNEL
Загружено: 2026-02-07
Просмотров: 26
Описание:
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda, ameishauri Serikali kuandaa Mpango wa kupanda miti Kata kwa Kata kwa kuwatumia vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa ili kutimiza azma ya kulinda na kuhifadhi mazingira kwa matokeo bora ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Mhe. Pinda ameyasema hayo alipokua akiongoza zoezi la upandaji miti lililoandaliwa na Taasisi ya Habari Conservation Organization (HCO) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwenye eneo la Chimwanga, Njedengwa Jijini Dodoma lenye ukubwa wa Ekari 72 leo Februari 06, 2026 zoezi ambalo pia limehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule.
“Tukichukua watendaji wa Kata na Mitaa, tunaweza ‘ku-organize’ vijana hawa na kazi ikawa nzuri tukiifanya kuwa ‘event’ ya kila mwaka, kila tunapopata miti ya kutosha, tunahama kutoka Kata hizi tunakwenda Kata zinazofuata, kwa sababu suala la umwagiliaji sio tatizo kwa miti 20 au 40 kwenye mstari mmoja, maji yapo, na mimi nipo tayari kuwa Championi wa hilo jambo”.
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, amesema Mkoa wake umeendelea na Kampeni mbalimbali za upandaji miti na kwa sasa kampeni inayoendelea ni upandaji wa miti ya matunda ili kuwapa motisha wananchi kupata faida za kivuli, chakula na uchumi hali inayoongeza mwamko wa kupanda miti hususan mti wa tunda la Tufaa.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Bw. Denis Simba amesema Mamlaka yake inashiriki kulinda na kuhifadhi mazingira kupitia Sheria mpya ya ununuzi wa Umma ya mwaka 2023/24 imeelekezwa ununuzi wote wa Umma ufanyike kidigitali ili kuondoa uchafuzi wa mazingira kupitia matumizi ya karatasi sambamba na kupunguza safari.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: