KIBWIKO/KIGUU: Sababu, Dalili, Matibabu, Kuzuia
Автор: WikiElimu
Загружено: 2026-03-02
Просмотров: 35
Описание:
Katika video hii inazungumza kuhusu sababu, dalili, matibabu, namna ya kuzuia, matarajio baada ya matibabu ya KIBWKO au KIGUU , endelea angalia mpaka mwisho kujifunza
Mtoto mwenye kibwiko au kiguu (clubfoot) anazaliwa na miguu au mguu wenye wayo uliogeukia ndani au nje. Hali hii inakuwepo mtoto anapozaliwa.
Kibwiko/kiguu ndio tatizo la miguu linaloathiri watoto wengi zaidi wakati wa kuzaliwa.
Ukubwa wa tatizo unatofautiana kati ya mtoto na mtoto – kuna wengine unakuta tatizo sio kubwa na miguu haijakaza – ila kuna wengine unakuta tatizo ni kubwa na miguu imekakamaa kabisa – inaweza kuwa ngumu hata kuinyoosha ikae sawa
Sababu ya kutokea kwa hali hii, haijulikani – lakini kuna uwezekano kwama linarithiwa ndani ya familia fulani.
Watoto wanaozaliwa kwenye familia yenye historia ya kuwa na kibwiko wanauwezako mkubwa zaidi wa kuwa na tatizo hili – hasa wanaume
Hali hii inampata mtoto 1 kati ya 1000 wanaozaliwa.
Utambuzi wa kibwiko/kiguu
Hali hii inatambuliwa kwa kufanya uchunguzi wa mwili pekee. Eksirei ya mguu inaweza kufanywa pia.
Uchaguzi wa matibabu ya kibwiko/kiguu
Kwa sababu hali hii inatambulika baada tu ya kuzaliwa – madaktari watakuelekeza matibabu yanayohitajika.
Mtoto anaweza kunyooshwa miguu ili kuiweka sawa na kisha kuishikiza kwa hogo ili usipinde tena. Mara nyingi shughuli hii inafanywa na daktari wa mifupa.
Matibabu yanapaswa kuanza mapema iwezekanavyo—hasa baada tu ya kuzaliwa—wakati huu ndio rahisi kunyoosha miguu.
• Kuivuta na kuionyoosha miguu polepole na kisha kuiwekea hogo kunafanyika kila wiki ili kuiweka miguu sawa. Kwa kawaida, mtoto anaweza kuwekewa hogo mara tano mpaka kumi hivi. Hogo la mwisho linaweza kukaa hapo kwa wiki 3. Baada ya mguu kukaa sawa, mtoto atapaswa kuvaa viatu maalum vyenye vishikiza (braces) kwa angalau miezi mitatu usiku na mchana. Kisha, ataendelea kuvivaa usiku pekee wakati analala kwa angalau miaka 3.
• Mara nyingi, shida inakuwa kwenye kano (tendon) za kisigino na upasuaji mdogo unaweza kuhitajika ili kuzilegeza kama zimekaza sana
• Kama tatizo ni kubwa sana, vusa vingine va kibwiko vinahitaji upasuaji ili kurekebika kama matibabu mengine yameshindwa au kama tatizo linajirudia.
• Mtoto anapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu na mtaalamu wa huduma za afya mpaka atakapokuwa mtu mzima.
Wakati gani utafute huduma ya matibabu kwa haraka?
Kama mwanao anayepatiwa tiba ana dalili zifuatzo- onana na daktari kama:
• Vidole vya miguu vimevimba au vimebadilika rangi baada ya kuwekewa hogo (cast)
• Kama hogo alilowekewa mtoto linasababisha maumivu makali – utaona mtoto Analia sana
• Kama vidole vimepotelea kwenye hogo/hogo limeteleza na kufunika vidole
• Kama hogo limeteleza na kuchomoka
• Kama wayo wa mguu umeanza kugeukia ndani tena baada ya matibabu.
Nini cha kutarajia mwanao akizaliwa na kibwiko?
Matokeo yanakuwa mazuri tu baada ya matibabu.
Emmanuel Mniko #mniko #wikielimu
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: