Huduma za afya Siaya kuimarika baada ya kaunti hiyo kusaini mkataba wa ushirikiano
Автор: KBC Channel 1
Загружено: 2026-02-05
Просмотров: 74
Описание:
AFYA BORA SIAYA
Huduma za kina mama na watoto katika kaunti ya Siaya zinatarajiwa kuimarika baada ya serikali ya kaunti kutia saini mkataba wa maelewano na shirika lisilo la serikali, Lwala Community Alliance. Afisa mkuu mtendaji wa shirika hilo Julius Mbeya amesema wametenga shilingi milioni 150 kufadhili uwekaji wa vifaa muhimu katika vituo vyote vya afya ya umma katika kaunti ya Siaya kwa madhumuni ya kupunguza vifo vya kina mama wanaojifungua kwa takriban asilimia 70. Makubaliano hayo ya miaka mitano pia yatafanikisha utoaji mafunzo kwa wahudumu kuhusu mbinu bunifu za huduma kwa kina mma. Gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo alisifia makubaliano hayo akisema yatapunguza gharama ya matibabu katika kaunti hiyo na akatoa wito kwa wahisani zaidi kujitokeza kupiga jeki sekta ya afya.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: / kbcchannel1tv
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: