RC RUVUMA AKABIDHI BAADHI YA MAHITAJI KWA WAATHIRIKA WA MAAFA SONGEA
Автор: RUVUMA RS
Загружено: 2026-01-28
Просмотров: 63
Описание:
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amekabidhi magodoro na mablanketi kwa kaya 27 zilizokumbwa na maafa ya mvua kubwa zilizoambatana na upepo mkali katika Kata ya Tanga, Halmashauri ya Manispaa ya Songea.
Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi mahitaji hayo, Brigedia Jenerali Ahmed amesema jumla ya wananchi 430 walipata athari kutokana na mvua hizo, na baadhi ya wadau wakiwemo Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania wamejitokeza kuwashika mkono waathirika.
Amesisitiza kuwa vifaa hivyo viwafikie walengwa husika na kuwataka wananchi kuwa na tabia ya kufuatilia taarifa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa ili kuchukua tahadhari mapema na kuepuka madhara yanayotokana na mvua kubwa na upepo mkali.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: