WAZIRI JERRY SILAA ATUA MBEYA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI KATI YA WANANCHI NA TARI ATOA MAAGIZO MAZITO
Автор: Site Tv Online
Загружено: 2023-11-23
Просмотров: 2681
Описание:
Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo ya makazi Mhe Jerry Silaa, ameagiza kufanyika haraka kwa tathmin ya wananchi waliopo katika eneo lenye ekari zaidi ya 60 katika mitaa ya Sae na Ituha jijini Mbeya, Ili walipwe fidia na Wizara ya kilimo kwaajili ya kuacha eneo hilo liendelee kubaki chini ya kituo cha utafiti wa Kilimo Tanzania TARI kituo cha Uyole jijini humo.
Silaa ameagiza tathmini hiyo ianze kufanyika kuanzia Jumamosi kwa wananchi ambao wako tayari kuthamini maeneo yao, ikiongozwa na mtathmini Mkuu wa Serikali pamoja na Kamishna wa ardhi nchini Ili kutoa nafasi kwa Wizara ya kilimo kulipa fidia kwa wananchi hao na kutoa nafasi kwa kituo cha utafiti kuendelea kukuza secta ya kilimo kupitia tafiti zinazofanywa na TARI.
Awali akiwasikisha taarifa kwa Waziri, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe Beno Malisa, amesema changamoto kubwa katika eneo hilo wamekua wakikwamisha kufikia mwafaka wa mgogoro huo, kutokana na kukataa kukaa pamoja kama walivyo agizwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa madai kwamba hawana muda huku wakiendelea na ujenzi wa nyumba katika eneo hilo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: