MSHINDE_MSHITAKI_WAKO
Автор: SHADAI TV
Загружено: 2026-01-29
Просмотров: 27
Описание:
MSHINDE MSHITAKI WAKO.
(1PETRO 5:8) Muwe na kiasi na kukesha; kwakuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama Simba angurumaye , huzunguka zunguka , akitafuta mtu ammeze.Maana ya kiasi na kukesha ni kukaa katika utakatifu , kwa sababu shetani kazi yake ni kutafuta sababu ya kuwashitaki watakatifu.
(AYUBU 1:6-12, 2:1-3) Ukisoma hapo unaona Ayubu alivochochewa na shetan ili atende dhambi , sura ya 1:10 unaona shetani akisema , Wewe hukumzingira Kwa wigo pande zote , pamoja na nyumba yake , na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia , nayo Mali yake imeongezeka katika nchi. Kwahyo kumbe shetani anachokua anatamani kwako ni utende dhambi Ili ulinzi wa Bwana uondoke ili apate uhalali wa kukutesa , hapo ni kwamba kulikua na ulinzi wa Mungu kwa Ayubu mpaka Mungu mwenyewe alivyomruhusu shetan amjaribu.Kwahyo kesha ukikaa katika utakatifu ili kumshinda mshitaki wako kama Ayubu pamoja na mateso yote hakumtenda Mungu dhambi ndio maana alishinda.
(ZEKARIA 3:1-4) Ukisoma hapa inaonesha Yoshua kuhani mkuu amesimama mbele ya Malaika wa Bwana na shetani akiwa amesimama mkono wake wa kulia akiwa ni mshitaki wake , vazi alilokua amevaa ambalo ni dhambi, Mpaka pale Malaika wa Bwana alivyosema mvueni nguo hizi chafu, Tazama nimekuondolea uovu wako , nami nitakuvika mavazi ya thamani kubwa.
(WAEFESO 5:27) Inasema;Apate kujiletea kanisa tukufu , lisilo na dosari Wala kunyanzi Wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
Maana yake Mtakatifu akifanya dhambi anakua mtuhumiwa , Kristo akirudi kunyakua kanisa hatochukua kanisa lenye lawama , shutuma ya uovu maana shetani ndiye mshitaki wetu halali huzunguka zunguka akimtafuta mtu ammeze.
(1YOHANA 2:1) Watoto wangu wadogo , nawaandikia haya ili msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu kristo mwenye haki.
Maana ya( Mwombezi )ni mtetezi wetu, Shetani ni mshitaki wetu ila Yesu ndiye Mtetezi wetu ambapo tutendapo dhambi , tukarudi kutubu kwa unyenyekevu Yesu anakua mtetezi wetu na Mungu anatusamehe.
(LUKA 22:31-32) Ukisoma hapa Yesu alikua akitabiri kuhusu Petro kumkana; Shetani alitumia andiko la ZEKARIA 13:7b ili kuwapata kondoo ambao n wanafunzi wa Yesu katika ulimwengu wa Roho pale Yesu alipoenda kupigwa msalabani ili awatawanye , Lakini Yesu alikua ameshawaombea ambaye ni Mtetezi wetu na kumshinda shetani ambaye ni mshitaki wetu.
JE UTAMSHINDAJE SHETANI?
(UFUNUO 12:10-11)
1.Utamshinda kwa Damu ya Yesu .
2.Utamshinda Kwa Ushuhuda wa maisha yako.( Hapa haimaanishi ushuhuda wa kumuhaibisha shetani mfano; namshukuru Mungu nimefaulu masomo, nimenunua kiwanja n.k, Ushuhuda unaoongelewa hapa ni kwamba wewe huna dhambi mbele za Mungu na mwanadamu kwa sababu shetani anatafuta Sababu kutokana na dhambi ili akutese.
Amina 🙏 mbarikiwe na Bwana.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: