Ujio wa Kiwanda: Wafugaji Misungwi wakabidhiwa Ng'ombe wa kisasa
Автор: BMG ONLINE TV
Загружено: 2018-05-04
Просмотров: 10846
Описание:
Mkuu wa Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, Juma Sweda amekabidhi madume tisa ya ng’ombe wa kisasa kwa wafugaji (wananchi) wa Kata za Misasi na Bujima kama mbegu kwa ajili ya kuwasaidia kuboresha mifugo yao.
Madume hayo yameboreshwa katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Mabuki na yameuzwa kwa wafugaji hao kwa bei ya ruzuku ya shilingi laki mbili kila mmoja ambapo gharama halisi ni kati ya shilingi laki sita hadi laki saba.
Akikabidhi madume hayo jana Mei 04, 2018, Sweda alisema lengo la serikali ni kuboresha maisha ya wananchi kwa kubadilisha mfumo wao wa maisha kwa kuwawezesha kujitegemea kiuchumi kupitia ufugaji wenye tija.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Misungwi, Eliurd Mwaiteleke alisema hatua hiyo ni mwanzo wa mikakati ya halmashauri hiyo kuanzisha kiwanda cha uchakataji maziwa kwani rasilimali maziwa ya kuendesha kiwanda hicho ipo na soko pia lipo.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Mabuki, Moses Ngendelo alisema lengo la kugawa madume hayo aina ya Nkole ni kuhakikisha wafugaji wanaboresha ufugaji wao kwa kufuga mifugo michache na yenye tija kupitia ufugaji wa ng’ombe wa maziwa pamoja na nyama.
Baadhi ya wafugaji waliopokea madume hayo walishukuru kwa fursa hiyo na kuahidi kuyatunza vizuri kwa ajili ya manufaa yao pamoja na ya wafugaji wengine na kwamba wamejifunza kushughulika na ufugaji wa kisasa na wenye tija.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: