BODI YA MIKOPO 'HESLB' WATANGAZA HILI KWA WANAFUNZI, 'KIWANGO CHA CHINI CHA MKOPO CHAONGEZEKA'
Автор: Millard Ayo
Загружено: 2024-09-29
Просмотров: 23814
Описание:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetangaza awamu ya kwanza ya wanafunzi walionufaika huku kiwango cha chini cha mkopo kwa mnufaika chaongezeka.
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk Bill Kiwia akizungumza na waandishi wa habari Septemba 28, 2024 amesema katika awamu ya kwanza wanafunzi 21,509 wamepangiwa mikopo.
Kwa mujibu wa Dk Kiwia katika mwaka huu kiwango cha chini cha mkopo kwa mnufaika mmoja mmoja kimepanda hadi Sh3 milioni kutoka Sh2.7 milioni mwaka uliopita wa 2023/2024.
“Hii inafanya wastani wa ada kiwango cha chini unaotolewa kufikia Sh530,000 kutoka Sh230,000, hela hii inawafanya sasa wanafunzi wanaosoma kozi za bei nafuu kuwa na uwezo wa kulipiwa karibu ada yote wanayopaswa kulipa,” amesema Dk Kiwia.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: