MAKAMBA MLIPUA LISSU BUNGENI, KUZUIA UCHAGUZI NI UHAINI, "NAUNGANA NA G55, NITAGOMBEA.....
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2025-04-10
Просмотров: 11291
Описание:
Mbunge wa Viti Maalumu, Salome Makamba amesema kauli zinazotolewa na viongozi wa Chadema kuhusu kuzuia uchaguzi, ni dalili za kushindwa huku akifananisha na watu walioweka mpira kwapani.
Makamba ametoa kauli hiyo leo Alhamisi April 10, 2025 bungeni wakati akichangia Hotuba ya Waziri Mkuu kwa Makadilio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/26 ambayo yaliwasilishwa na Waziri Kassim Majaliwa jana.
Makamba ni miongoni mwa wabunge 19 wa Chadema ambao wamekuwa na mgogoro ndani ya chama chao baada ya kudaiwa kuwa walijipeleka na kula kiapo bila ruhusa ya chama hicho.
Mbunge huyo amesema hakuna mwenye uwezo wa kuuzuia uchaguzi na kwamba anaungana na wanachama 55 wa Chadema waliosema lazima uchaguzi ufanyike (maarufu G55).
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: