MAFANIKIO SEKTA YA AFYA, HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA CHATO
Автор: Wizara ya Afya Tanzania
Загружено: 2025-10-16
Просмотров: 134
Описание:
CHATO - GEITA
Katika kipindi cha miaka minne pekee, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato imeibuka kuwa kielelezo cha mageuzi makubwa katika sekta ya afya nchini kutoka ndoto hadi uhalisia. Uwekezaji huu umeifanya hospitali hii kuendelea kwa kasi na kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja.
Chato RRH sasa inajivunia miundombinu bora, vitendanishi vya kisasa, huduma za kibingwa na ubingwa bobezi, sambamba na ongezeko la huduma za vipimo na upatikanaji wa dawa kwa wakati. Ufanisi huu umechangia kupungua kwa muda wa matibabu, huku wananchi wakipata huduma zenye ubora wa hali ya juu katika mazingira rafiki na salama.
Serikali pia imeendelea kuimarisha rasilimali watu kwa kuongeza ajira mpya za watumishi wa afya, ili kuhakikisha kila mgonjwa anahudumiwa kwa wakati, kwa uangalizi na kwa upendo.
Chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato imegeuka kuwa nguzo ya tiba bora, matumaini na ubunifu wa kiafya kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa.
Fuatilia makala hii maalum kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Afya, inayobainisha hatua kwa hatua safari ya mafanikio ya Chato ZRH katika kuboresha huduma za afya nchini.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: