Kishindo cha bondia Hassan Mwakinyo chatua bungeni, kila mbunge atoa Tsh. 20,000
Автор: Azam TV
Загружено: 2018-09-14
Просмотров: 43189
Описание:
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania wamekubaliana kila mmoja kutoa kiasi cha shilindi 20,000 kwaajili ya kumpongeza bondia Hassan Mwakinyo kwa kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania barani Ulaya.
Bondia huyo mwishoni mwa wiki iliyopita alimtwanga bondia Sam Eggington wa Uingereza kwa KO raundi ya pili katika pambano la utangulizi kuelekea pambano kati ya Amir Khan na Samuel Vargas lililofanyika kwenye ukumbi wa Arena Birmingham nchini England.
Bondia huyo leo alikuwa ni sehemu ya wageni waliohudhuria kikao cha mwisho cha mkutano wa 12 wa Bunge, ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika hotuba yake ya kuahirisha Bunge, amempongeza Mwakinyo kwa kuitangaza vyema Tanzania Kimataifa.
Mara baada ya pongezi hizo, mbunge wa Sumbawanga Mjini Aeshi Hilaly akatoa hoja ya wabunge wote kumpongeza bondia huyo kwa kumchangia shilingi 20,000 kila mmoja, hoja ambayo iliungwa mkono na wabunge wote.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: