ycliper

Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
Скачать

TAFAKARI YA SIKU ALHAMISI YA JUMA LA 3 MWAKA C 31/01/2019

Автор: KANISA KATOLIKI TANZANIA TEC

Загружено: 2019-01-30

Просмотров: 1619

Описание: #Mt.YohaneBosko
WAPENDWA TAIFA LA MUNGU TUMSIFU YESU KRISTO!
KARIBUNI KATIKA TAFAKARI YA SIKU: TAREHE 31/01/2019
(Alhamisi ya Juma la 3 la Mwaka) KUMBUKUMBU YA MT. YOHANE BOSKO
WAZO KUU: KUTENDA MEMA
SOMO LA INJILI ILIVYOANDIKWA NA MT. MARKO 4:21 – 25
Akawaambia, “Mwaonaje? Taa huja ili kuwekwa chini ya pishi, au mvunguni? Si kuwekwa juu ya kiango? Kwa maana hakuna neno lililositirika, ila makusudi lije likadhihirika; wala hakuna lililofichwa ila makusudi lije likatokea wazi. Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.” Akawaambia, “Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakacho pimiwa, na tena mtazidishiwa. Kwa maana mwenye kitu atapewa, naye asiye na kitu, hata kile alichonacho atanyang’anywa.”
NENO LA BWANA…
Wapendwa Taifa la Mungu!, katika Injili tuliyoisikia hivi punde, Bwana wetu Yesu Kristo anatufundisha sisi tulio wafuasi wake, kwa sacramenti ya Ubatizo tumepewa wajibu wakutekeleza, yaani kuweka taa juu ya kiango ili kuumulika ulimwengu wenye giza. Anatumia neno taa yaani Mwanga akimaanisha Neno la Mungu, kama Mzaburi anvyotufundisha “Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga wa njia yangu” (Zab 119:105).
Pia Neno Mwanga lina mwakilisha Kristo mwenyewe kama anavyo jitambulisha “Mimi ndimi nuru ya ulimmengu yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe” (Yn 8:12) hayo ni maneno yake Kristo tunayo ambiwa, kusudi tupate kufuata mwenendo wake na desturi zake tukitaka kweli kuweka taa juu ya kiango. Basi bidii yetu kubwa sharti iwe kujifunza maisha ya Yesu kristo aliye Nuru ya Ulimwengu.
Kwa kawaida taa ikiwekwa mvunguni giza hutawala, vivyo hivyo Neno la Mungu lisipo dhihirika, giza hutawala, giza linalo maanishwa hapa ni dhambi na mizizi yake.
Wapendwa Taifa la Mungu, Ulimwengu wa leo unahitaji kuangazwa ili kuondoa giza la dhambi hasa katika ngazi ya Familia ambayo ni shule ya malezi msingi kwa mwanadamu: kunaweza kuwapo magomvi, kutoaminiana, kuhisiana vibaya, na kusemana ovyo mitaani. kuzembea katika kutimiza wajibu zetu hasa wazazi katika jukumu la malezi kwa kisingizio cha kazi nyingi. Tabia za waume kuwatesa wake zao na baadhi ya wake kuwatesa waume zao. Je! sio kuweka taa mvunguni huko?
Katika jamii tunamoishi kuna giza la dhambi giza hilo ni matendo ya: uuwaji wa vikongwe, uuaji wa mimba, wizi wa aina mbalimbali kwa mfano: Vitendo vya rushwa, kuhujumu uchumi na ufisadi. Pia kuna dhambi ya uharibifu wa mazingira yaani “Nyumba ya wote” kama tunavyo fundishwa katika waraka wa kitume ‘Laudato Si’ wa Baba Mt. Francisko. Je! Mambo kama hayo sio kuweka taa mvunguni?
Wapendwa Taifa la Mungu, tunaalikwa kuachana na vitendo vya giza kwa maana “…zamani ninyi mlikua giza, bali sasa mmekua nuru katika Bwana enendeni sasa kama watoto wa nuru” (Eph 5:8).
Hivyo sisi tuliowafuasi wa Kristo kwa njia ya ubatizo, tunaagizwa kutangaza neno la Mungu, tuchangie kuleta mwanga wa hali Njema katika Familia ya mwanadamu na jamii inayotuzunguka ili kuweka taa juu ya kiango yaani kulidhihirisha neno la Mungu kwa kulitangaza na kuliishi.
➢ Angalieni msikialo: yaani tutilie maanani yale tunayosikiliza, yatusaidie kuzaa matunda mema.
➢ Angalieni kipimo kile mpimacho ndicho mtakacho pimiwa: kwamba kadiri tunavyo fanya jitihada kulisikiliza Neno la Mungu na kuliishi kadiri hiyohiyo tunapata msaada wa neema ya Mungu.
➢ Wapendwa Taifa la Mungu, tumuombe Mungu atujalie bidii ya kusikiliza na kutenda mapenzi yake, hivyo tuweke Taa juu ya kiango ili watu wayaone matendo yetu mema na wamtukuze Mungu.

TAFAKARI HII IMETOLEWA KWENU NA FRT. DAUDI MAKUNGU WA JIMBO KATOLIKI SUMBAWANGA, MWAKA WA TATU WA TEOLOJIA KATIKA SEMINARI KUU KIPALAPALA - TABORA

Не удается загрузить Youtube-плеер. Проверьте блокировку Youtube в вашей сети.
Повторяем попытку...
TAFAKARI YA SIKU ALHAMISI YA JUMA LA 3 MWAKA C 31/01/2019

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио

Похожие видео

KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH : IBADA YA EVENING GLORY - THE SCHOOL OF HEALING - 05/02/2026

KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH : IBADA YA EVENING GLORY - THE SCHOOL OF HEALING - 05/02/2026

Askofu Mkuu Ruwa'ichi Hapa Duniani sisi n wapita njia Ishi kama ndiyo siku ya Mwisho Padre Sabuni

Askofu Mkuu Ruwa'ichi Hapa Duniani sisi n wapita njia Ishi kama ndiyo siku ya Mwisho Padre Sabuni

Почки скажут вам: всего 1 стакан перед сном и ночные походы в туалет исчезнут | ПАМЯТЬ И МОЗГ

Почки скажут вам: всего 1 стакан перед сном и ночные походы в туалет исчезнут | ПАМЯТЬ И МОЗГ

Huyu ndiye Mtunzi wa wimbo

Huyu ndiye Mtunzi wa wimbo "Lala Kitoto cha Mbingu"

Ibada Ya Morning Glory,  Ijumaa,  06 .02  . 2026.

Ibada Ya Morning Glory, Ijumaa, 06 .02 . 2026.

#LIVE:MISA TAKATIFU YA KILA SIKU ASUBUHI PAROKIA YA BIKIRA MARIA MSAADA WA DAIMA KIMARA KOROGWE DSM

#LIVE:MISA TAKATIFU YA KILA SIKU ASUBUHI PAROKIA YA BIKIRA MARIA MSAADA WA DAIMA KIMARA KOROGWE DSM

KHAMENEI AMEMWAMBIA TRUMP UKWELI!

KHAMENEI AMEMWAMBIA TRUMP UKWELI! "MAJESHI YAKO NI YA KIGAIDI" UCHAFU WA USA NA ISRAEL UMEFICHUKA

Wosia wa Marehemu Padre Sabuni, ulivyosomwa na Mwanadarasa wake Padre Aidan Mubezi Misa ya Mazishi

Wosia wa Marehemu Padre Sabuni, ulivyosomwa na Mwanadarasa wake Padre Aidan Mubezi Misa ya Mazishi

Sona Shahgeldyan & Garnik Yeghiazaryan / Qez het qeznov (Official Music Video 2026)

Sona Shahgeldyan & Garnik Yeghiazaryan / Qez het qeznov (Official Music Video 2026)

Сила Утреннего Ритуала Определяет Весь Твой День | Наполеон Хилл

Сила Утреннего Ритуала Определяет Весь Твой День | Наполеон Хилл

Maneno ya mdogo wake Padre Paul Sabuni yalivyogusa watu katika Misa ya Mazishi/ Afananishwa na Padre

Maneno ya mdogo wake Padre Paul Sabuni yalivyogusa watu katika Misa ya Mazishi/ Afananishwa na Padre

UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA MIAKA 40 YA HOSPITALI YA KARDINAL RUGAMBWA, UKONGA - DAR ES SALAAM

UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA MIAKA 40 YA HOSPITALI YA KARDINAL RUGAMBWA, UKONGA - DAR ES SALAAM

Hivi ndivyo Mapadre wanavyomkumbuka Marehemu Padre Paul Sabun/ Alikuwa na vipaji vingi/ Tunamshukuru

Hivi ndivyo Mapadre wanavyomkumbuka Marehemu Padre Paul Sabun/ Alikuwa na vipaji vingi/ Tunamshukuru

INJILI NA TAFAKARI SIKU YA DOMINIKA YA 26 MWAKA B WA KANISA

INJILI NA TAFAKARI SIKU YA DOMINIKA YA 26 MWAKA B WA KANISA

"Tuweke alama za kudumu kwa watu tunaoishinao" Askofu Musomba

Утренние молитвы Оптина Пустынь Молись о том, кого любишь! Начни день с молитвы!

Утренние молитвы Оптина Пустынь Молись о том, кого любишь! Начни день с молитвы!

"Nitume mimi Bwana." Kwaya ya Mafrateli wa Shirika la Karmeli Tanzania.

EE MARIA UWAKUMBUKE MAREHEMU WOTE NA FR NTAPAMBATA II MISA YA MAZISHI PADRE PAUL SABUNI PUGU DSM

EE MARIA UWAKUMBUKE MAREHEMU WOTE NA FR NTAPAMBATA II MISA YA MAZISHI PADRE PAUL SABUNI PUGU DSM

LIVE:MWIGULU AKABIDHI HUNDI YA SH BIL 200 ZA UWEZESHAJI WA VIJANA/ TMA YATAHADHARISHA MVUA ZA MASIKA

LIVE:MWIGULU AKABIDHI HUNDI YA SH BIL 200 ZA UWEZESHAJI WA VIJANA/ TMA YATAHADHARISHA MVUA ZA MASIKA

#LIVE: MISA TAKATIFU YA MAZISHI YA MAREHEMU PADRE PAUL SABUNI - KITUO CHA HIJA PUGU JIMBO KUU LA DSM

#LIVE: MISA TAKATIFU YA MAZISHI YA MAREHEMU PADRE PAUL SABUNI - KITUO CHA HIJA PUGU JIMBO KUU LA DSM

© 2025 ycliper. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]