BEI YA SIMENTI YAFIKIA 24,875/=, NONDO NA MABATI YATAJWA,WAZIRI AFUNGUKA
Автор: Millard Ayo
Загружено: 2023-07-25
Просмотров: 3497
Описание:
Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji akitoa maelezo kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa muhimu za chakula na za viwandani kwa mwezi Julai 2023 ambapo amesema bei ya saruji (aina ya 32.5 R) imeongezeka kutoka Shilingi 23,125 kwa bei ya juu mwezi Juni hadi Shilingi 23,250 na bei ya chini ni shilingi 14,125 kutoka shilingi 13,500 kwa mfuko wa kilo 50 huku bei za Nondo na Bati zikionesha kuwa himilivu.
“Saruji aina ya 32.5 kwa mwezi Julai 2023 ni kati ya Shilingi 14,125 na 23,250 kwa mfuko wa kilo 50. Bei ya juu ya saruji hiyo imeongezeka kwa asilimia 0.5 sawa na ongezeko la Shilingi 125 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na bei ya mwezi Juni 2023 ambayo ilikuwa ni Shiling 23,125 kwa mfuko wa kilo 50. Vilevile, bei ya chini ya saruji imeongezeka kwa asilimia 4.6 sawa na ongezeko la Shilingi 625 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na bei ya mwezi Juni 2023 ambayo ilikuwa ni Shilingi 13,500 kwa mfuko wa kilo 50 na Mkoa wenye bei ya chini ni Tanga, wakati bei ya juu ipo katika mkoa wa Kagera. Aidha, uchambuzi wa wastani wa bei ya saruji (aina ya 32.5) nchini unaonesha kuwa bei yake imepanda kwa asilimia 3.2 ukilinganisha na wastani wa bei ya bidhaa hiyo kwa mwezi Juni 2023” Waziri wa Viwanda na biashara Dkt. Kijaji.
“Kwa saruji (aina ya 42.5), uchambuzi unaonesha kuwa bei kwa mwezi Julai 2023 ni kati ya Shilingi 15,000 na 24,875 kwa mfuko wa kilo 50. Bei ya juu ya saruji hiyo imeongezeka kwa asilimia 1.5 sawa na ongezeko la Shilingi 375 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na bei ya mwezi Juni 2023 ambayo ilikuwa ni Shiling 24,500 kwa mfuko wa kilo 50. Halikadhalika, bei ya chini ya saruji ya aina hii imeongezeka kwa asilimia 2.4 sawa na ongezeko la Shilingi 350 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na bei ya mwezi Juni 2023 ambayo ilikuwa ni Shilingi 14,650 kwa mfuko wa kilo 50. Mkoa wenye bei ya chini ni Tanga, wakati bei ya juu ipo katika mkoa wa Kagera. Aidha, uchambuzi wa wastani wa bei ya saruji (aina ya 42.5) nchini unaonesha kuwa bei yake imepanda kwa asilimia 1.4 ukilinganisha na wastani wa bei ya bidhaa hiyo kwa mwezi Juni 2023” Dkt. Ashatu Kijaji Waziri wa Viwanda na Biashara.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: