MAKAMO WA PILI
Автор: Bahari Online TV
Загружено: 2026-02-27
Просмотров: 49
Описание:
Sikiliza Bahari FM Radio 97.5 Unguja | 91.1 Pemba
-----
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo umesaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na upatikanaji wa huduma mbali mbali za kijamii.
Ameyasema hayo katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo kwa wabunge wa CCM wa Zanzibar pamoja na wakuruenzi wa Halmashauri za Unguja na Pemba yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Amesema kukutana pamoja kwa wabunge wa CCM Zanzibari kunatoa fursa ya kutoa maoni yao na kujadili namna bora ya kuifanyia marekebisho sheria ya Mfuko wa Jimbo ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha Mhe. Hemed amewataka wabunge na watendaji wa Halmashauri kuondoa kasoro na vikwazo vilivyopo na kuweka mazingira rafiki ya utendeji wa kazi hasa kaika utekelezaji wa miradi ya maendeleo majimboni.
Amesema kuwa dhamira ya dhati ya Serikali ni kuhakikisha kuwa Mfumo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo unakuwa ni wenye tija na unaotekelezeka ambapo Sheria na miongozo yake lazima inaendane na hali halisi ya utekelezaji wenye uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika matumizi ya fedha za Umma.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Halmashauri zake zitaendelea kufanya kazi na wabunge katika kuhakikisha fedha za mfuko wa maendeleo ya Jimbo zinatumika kama ilivyopangwa na kuleta tija kwa wananchi wote.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed amewataka wabunge kushirikiana, kusaidiana na kuheshimiana jambo litakalopelekea kufikia malengo ya kuwaumikia na kuwasemea wananchi wa majimbo yao.
Ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha wanashiriki vyema kwa kujifunza, kujadiliana kwa kina, kubadilishana uzoefu na kutoa maoni yeo kwa uwazi ambayo yatapelekea kuujenga mfumo unaheshimu misingi ya utawala bora, kulinda rasilimali za umma na kutoa fursa sawa kwa Majimbo yote.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Muungano na Mazingira Muhandisi Hamad Yussuf Masauni ambae ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wabunge wa CCM Zanzibar amesema lengo la kufanyika kwa mafunzo hayo ni kupata maoni ya wabunge wa Zanzibar ambayo yatasaidia katika kuifanyia marekebisho na maboresho sheria ya Mfuko wa kuchochea maendeleo ya Jimbo.
Mhandisi Masauni ameeleza kuwa Mfuko wa jimbo umekuwa ni nyenzo Imara ya kuchochea maendeleo na kutoa msukumo wa kufanya kazi kwa uwazi, uaminifu na ubunifu katika kutekeleza miradi ya maendeleo majimboni.
Aidha, amesema mafunzo hayo yataimarisha zaidi mahusiano kati ya wabunge na watendaji wa Halmashauri katika kufanya kazi zao ili kupunguza urasimu wa upatikanaji wa fedha za Mfuko wa kuchochea maendeleo ya Jimbo.
Nae katibu wa Umoja wa wabunge wa CCM Zanzibar Mhe. Zainab Abdalla Issa amesema wabunge wa Zanzibar wataendelea kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano katika kuwahudumia wananchi wa Zanzibar pamoja na kuzielezea kazi kubwa zinazofanywa na viongozi za kuwaletea wananchi maendeleo.
Mhe. Zainab amesema upo umuhimu wa kuipitia upya sheria na Sera ya Serikali za mitaa ili ushiriki wa wabunge ndani ya Halmashauri uwe wa lazima ambao uawapa nafasi ya kusimamia vyema matumizi ya fedha za miradi na kuhakikisha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: