GARI LAKAMATWA LIKISAFIRISHA VYUMA CHAKAVU BILA KIBALI
Автор: TBConline
Загружено: 2020-07-22
Просмотров: 492
Описание:
GARI LAKAMATWA LIKISAFIRISHA VYUMA CHAKAVU BILA KIBALI
Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na jeshi la polisi mkoani Pwani limekamata gari lenye namba T666CSC likiwa limebeba malighafi za chuma chakavu zaidi ya tani kumi likitokea jijini Mbeya kuelekea katika kiwanda cha youn stee kilichopo Kibaha mkoani Pwani bila kibali cha kusafirishia vyuma hivyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa (NEMC) kanda ya mashariki bwana Arnold Mapinduzi amesema kibali cha kusafirisha vyuma chakavu kinatolewa na waziri mwenye dhamana ya mazingira.
Mapema waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mussa Azan Zungu baada ya kufika kituo cha polisi oysterbay ambapo gari hiyo imeifadhiwa ameagiza nemc kufuata sheria zote zinazotakiwa.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: