Mshindi wa Nembo ya ZRA Atangazwa
Автор: ZRA ONLINE TV
Загружено: 2023-03-17
Просмотров: 1393
Описание:
Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) imemtangaza ndugu Hussein Hamis Hussein kuwa mshindi wa shindano la ubunifu wa nembo rasmi itakayoitambulisha taasisi hiyo.
Mshindi huyo alitangazwa leo katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Nembo hiyo, liyofanyika katika Afisi za Makao Makuu ya ZRA Mazizini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar ndugu Yusuph Juma Mwenda alisema uteuzi wa Nembo hiyo umezingatia mambo mengi ikiwemo kutenda haki na usawa kwa walipakodi wote.
Aliongeza kuwa, ni malengo ya uanzishwaji wa ZRA kusimamia na kutoa huduma bora kwa wadau wote, hivyo, nembo hiyo inaendelea kutoa ahadi ya taasisi kwa wadau kuwa haki itaendelea kutendeka na huduma bora zitachukua nafasi yake.
Kamishna Mwenda alisema mabadiliko ya nembo yatachochea ari na utendaji wa ZRA kwa kuwa ni sehemu ya ahadi yao kwa walipakodi.
Mapema akizungumzia mchakato wa kupata nembo hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya kuhamia ZRA ndugu Mohammed Amour Mohammed alisema jumla ya wabunifu 60 waliwasilisha Nembo 75 ambazo zilifanyiwa mchujo na kupatikana nembo hiyo moja ambayo imetangazwa leo.
Alibainisha kuwa, utaratibu wa kupata Nembo mya ya ZRA ni suala la kisheria kama ilivyoainishwa na katika kifungu cha nne cha Sheria ya Uanzishwaji wa ZRA ya mwaka 2022.
Naye Mshindi wa shindano hilo Ndugu Hussein Hamis Hussein alius ukuru uongozi wa ZRA kwa kuichagua kazi yake katika kazi 75 zilizowasilishwa, na akawaomba wabunifu wachanga wasichoke kutumia kila fursa itakayojitokeza.
Mshindi wa Shindano hili alikabidhiwa kitita cha Shilingi milioni 3 kama zawadi kwa ubunifu wake huo.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: