Shabiby ataka laini za simu zichangie Bima ya Afya kwa wote, hospitali za Serikali zibinafsishwe
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2024-04-05
Просмотров: 780
Описание:
Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby ameshauri kila mwenye simu akatwe Sh2,000 kila mwezi, wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi wakatwe Sh10,000 na hospitali, zahanati na viuto vya afya vya Serikali vibinafsishwe.
Shabiby amesema hayo leo Ijumaa Aprili 5, 2024 wakati akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Amesema kuna wamiliki wa laini za simu nchini milioni 72 ambao makato yao kwa mwaka yataingiza Sh1.720 trilioni na zikijumlishwa za Sh10,000 kwa mwezi za wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi Serikali itapata kwa mwaka takriban Sh2 trilioni, zitasaidia kuwa chanzo cha mapato ya uhakika kwa Bima ya Afya kwa wote.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: