UJENZI WA BWAWA LA KIDUNDA WAFIKIA ASILIMIA 40, TATIZO LA MAJI DAR LINAELEKEA KUMALIZIKA
Автор: Jamii focus
Загружено: 2025-12-16
Просмотров: 198
Описание:
UJENZI WA BWAWA LA KIDUNDA WAFIKIA ASILIMIA 40, TATIZO LA MAJI DAR LINAELEKEA KUMALIZIKA
Ujenzi wa Bwawa Kubwa la Kuhifadhi Maji la Kidunda, linalotekelezwa mkoani Morogoro, umefikia asilimia 40 ya utekelezaji, hatua inayotoa matumaini mapya ya kumaliza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Bwawa hilo linatarajiwa kuhifadhi zaidi ya lita bilioni 190 za maji, huku likigharimu zaidi ya shilingi bilioni 335, na linapangwa kukamilika mwaka 2026.
Mradi huo wa kimkakati unalenga kuimarisha upatikanaji wa maji kwa matumizi ya binadamu, viwanda na shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi, sambamba na kusaidia Taifa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Akizungumza baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati ili kuondoa kabisa tatizo la maji kwa wakazi wa Dar es Salaam, Pwani na maeneo jirani.
Aweso amesisitiza kuwa ulinzi wa vyanzo vya maji na mazingira yanayozunguka bwawa hilo ni jambo la msingi ili kuhakikisha bwawa linajaa maji mara baada ya kukamilika na linaendelea kuwa endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, amesema mradi wa Bwawa la Kidunda ni fursa kubwa ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmassi, ameeleza kuwa usimamizi madhubuti wa vyanzo vya maji na ushirikiano wa wananchi ni nguzo muhimu ya mafanikio ya mradi huo mkubwa wa kimkakati.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: