WAZIRI BASHUNGWA AMBANA MKANDARASI CHICO, UCHELEWESHWAJI WA MIRADI
Автор: Wizara ya Ujenzi
Загружено: 2024-01-22
Просмотров: 5647
Описание:
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Mb), amemuagiza Mkandarasi wa kampuni ya CHICO anayejenga barabara ya Makutano ya Ntyuka - Mvumi - Makutano ya Kikombo yenye urefu kilometa 76 na Barabara ya Chololo - Mapinduzi (Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi - TPDF) yenye urefu wa kilometa 5, kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi huo unapiga hatua katika utekelezaji wake ifikapo mwishoni mwa mwezi wa pili.
Akizungumza jijini Dodoma, Waziri Bashungwa, amemuagiza Mkandarasi huyo kuhakikisha kuwa anamaliza ujenzi wa sehemu ya barabara ya Kikombo - Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi - TPDF (Km 16), katika kipindi kilichopangwa.
Повторяем попытку...
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео
-
Информация по загрузке: